SIMU.TV: Waandishi wa habari jijini Dar es Salaam wameiomba kamati ya bunge huduma na maendeleo ya jamii kuwapa muda wa kuupitia muswada wa habari na kutoa maoni yao kabla ya kupitishwa na bunge. https://youtu.be/7r6qScPR0Yw
SIMU.TV: Makamu wa rais Samia Suluhu Hassani amepiga marufuku uharibifu wa mazingira unaoendelea sehemu mbalimbali nchini unaoweza kupelekea nchi kuwa jangwa. https://youtu.be/9pGimrqPpzU
SIMU.TV: Uharibifu mkubwa wa mazingira pamoja na uchomaji wa misitu ovyo umetajwa kuwa changamoto inayopelekea mabadiliko ya nchi maeneo mbalimbali. https://youtu.be/RKbzEUXEIeI
SIMU.TV: Halmashauri ya manispaa ya Ilala kesho inaanza rasmi kuwaondoa wafanyabiashara wanaofanya biashara kando kando ya barabara za magari yaendayo haraka. https://youtu.be/xFMSVW58DJE
SIMU.TV: Jeshi la polisi kanda maalumu ya Dar es Salaam linalitafuta kundi la matapeli lililotumia jina la mkuu wa mkoa Paul Makonda kutapeli kampuni ya Kichina https://youtu.be/Vn9x9rVQ7Ug
SIMU.TV: Rais wa Korea ya Kusini amemtunuku nishani ya heshima aliyekua mkuu wa wilaya ya Mkuranga Henry Clemence kwa kutambua jihada zake katika kuleta maendeleo kwa kutumia mfumo wa SMU. https://youtu.be/v0tPp8mNcS0
SIMU.TV: Mafundi wanaotumia saruji ya Rhino kuzalisha matofali jijini Mbeya wameiomba kampuni hiyo kujenga kiwanda katika mkoa wa Mbeya. https://youtu.be/R55Bdry3MiU
SIMU.TV: Vijana wa mkoa wa Dar es Salaam wametakiwa kujiunga na programu ya jiandalie ajira ili waweze kupata mafunzo ya ujasiriamali kwa ajili ya kuanzisha biashara zao. https://youtu.be/vNk5FoBUUts
SIMU.TV: Maziko ya bondia wa ngumi za kulipwa Thomas Mashali yatafanyika siku ya Jumatano tarehe mbili Novemba katika makaburi ya Kinondoni jijini Dar es Salaam. https://youtu.be/22oxZi-8yus
SIMU.TV: Tamasha kubwa la utamaduni maarufu kama Cha kale Dhahabu linatarajiwa kufanyika jijini Dar es Salaam December 30 katika uwanja wa Uhuru. https://youtu.be/TZXsRDxGnzk
SIMU.TV: Msanii chipukizi wa muziki wa kizazi kipya Rajabu Said ameibuka mshindi katika shindalo la Club Raha Leo Show. https://youtu.be/0Vx2jIoYovY
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...