KWA mara ya kwanza katika historia ya Muziki Tanzania,  Efm Radio inakuletea mkazi wa jiji la Dar es salaam, Tamasha kubwa, litakalowakutanisha wasanii wa muziki wa Singeli Tanzania nzima  ambapo zaidi ya wanamuziki 100 wa singeli wataperfom katika jukwaa moja pale Dar live, Mbagala Zakhiem octoba 14, 2016. Kuanzia kumi kamili jioni hadi kuchee.

 Efm redio itahakikisha mashabiki wa muziki huo wa singeli wanaburudika pamoja na wanamuziki wa muziki huu wa singeli kutambulika Tanzania nzima.

Unaacha buku  tano tu mlangoni na kushuhudia wakali wote wa singeli Tanzania wakiperfom akiwepo Dogo Nigga, Sholo Mwamba, Dula Makabila, Msaga sumu, Eskide Virus, Majid Migoma, Mc Miduku, Maseke,  Kaja kaka Mpemba, Machupa, Msaga Lami, Segu Segumbo, Makaveli na wengine kibaoo.

Vilevile tamasha hili litaenda sanjari na semina kwa wasanii wote wa singeli hasa chipukizi ambapo watoa mada watakuwa ni kutoka BASATA, TCRA,TRA na Mgeni rasmi kwa ajili ya ufunguzi wa semina hiyo anatarajiwa kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni sanaa na Michezo, Profesa Elisante Ole Gabriel Mollel.

Lengo ni  kuwafundisha maadili, jinsi ya kulipa kodi, na ni jinsi gani wataendeleza kazi zao kwa kujenga mahusiano mazuri na Taasisi hizo za Serikali.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...