Na  Bashir  Yakub.

Kurasimisha  biashara  kunazo  namna  nyingi.  Kufungua  kampuni   ni  moja  ya  namna  ya  kurasimisha  biashara. Kusajili  jina  la  biashara  nayo  ni  namna nyingine  ya  kurasimisha  biashara. Makala  yatazungumzia  hii  ya  pili  ya  kusajili  jina  la  biashara. Na  hii  ni  kwasababu  hii  ni  njia  nyepesi,  ya  haraka, na  ya gharama  ndogo  sana.

 Mfano  wa jina  la biashara  ni kama,   HK  bazaar, kinondoni  investment, Congo traders, Karoli  LTD  na  mengine  yanayofanana  na  hayo.

1.NINI  MAANA YA  JINA  LA  BIASHARA.
Jina  la  biashara  ni  lile  jina  linalotumiwa  na  mtu  kama  jina  la  utambulisho  wa  biashara  yake  inayofanywa  katika  mfumo  ambao  sio  kampuni.  Makampuni  yana  majina  lakini  majina  hayo  hayawezi  kuitwa  majina  ya  biashara  bali  ni  majina  ya  kampuni.

Jina  la  biashara  ni  kwa  yule  ambaye  biashara  yake  imesajiliwa   lakini  sio  kampuni.  
Aidha mwenye  biashara  ambayo  haijasajiliwa  lakini  analo  jina  fulani  analotumia  kisheria  huyo  hana  jina  la  biashara.Hilo  jina  sio  lake  na  mtu  mwingine  anaweza  kulisajili na  akamtaka  huyu  ambaye  hajalisajili  kuacha mara  moja  kulitumia . 
Ili  sheria  ikutambue  kuwa  una  jina  la  biashara   ni  pale  tu  unapokuwa   umesajili  jina  hilo.  

2. WAPI  WAWEZA  KUSAJILI  JINA  LA  BIASHARA.
Jina  la  biashara  husajiliwa  kwa  msajili  wa  biashara  na  makampuni ( BRELA). Ukifika   hapo  utawaeleza  kuwa  unataka  kusajili  jina  la biashara  watakupa  fomu  maalum  utaijaza .  Lakini  kabla  ya  hapo  utatakiwa   utume  maombi  maalum  hapohapo BRELA ukitaka  kujua  iwapo  jina  ulilochagua  kuwa  la  biashara   yupo  mtu  mwingine  analitumia au  lah.

Hii  ni  kwasababu  jina  ni  moja  Tanzania  nzima.  Hakuwezi  kuwa  na  majina  mawili  au  zaidi   yanayofanana  huku  yote  yakiwa  yamesajiliwa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...