TANZANIA COMMUNITY ORGANIZATION  
OF NORTHEN CALIFORNIA (TCO)  
912 Bayview Ave, Oakland, CA 94610  
510.290.9708, 510.472.7672 

Ndugu Watanzania na marafiki wa Northern California. 
Mwaka huu tutakuwa na fundraising nyingine ambayo itaambatana na kusheherekea kumbukumbu ya sherehe zetu za uhuru hapo Dec 10 2016.  Fundraising ya mwaka huu itakuwa ni kusaidia  vifaa/kifaa kwa zahanati (clinic) mojawapo kutoka kijiji kimojawapo Tanzania. 
Lakini kabla ya yote ni vizuri tuwape taarifa kwa ufupi juu ya juhudi zenu mlizofanya mwaka jana za kuwezesha kuchangia msaada wa ndugu zetu wenye ulemavu wa ngozi (albino)

Shughuli ilifanyika Dec 19 2015 katika mji wa Oakland - CaliforniaKatika mapato yaliyopatiakana basi Umoja wetu (TCO) uliweza kusaidia shule ya msingi ya Buhangija ambayo ni shule ya albinos  inayosaidia kuwasomomesha watoto hawa katika mazingira ya amani baada ya matukio ya kukatwa viungo kuwa mengi miaka michache iliyopita. 
TCO (Tanzania Community Organization) kupitia michango yenu iliweza kusaidia kiasi cha milioni 6, tisini na saba elfu (tsh 6,097,000)
Kiasi hiki kilitumwa kupitia kwenye serikali ya wilaya kwa kushirikiana na uongozi wa shule ili kuhakikisha msaada uliwafikia walengwa.Matumizi yake yalikuwa kama ifuatavyoWanafunzi waliweza kusaidiwa : 
1.Mashuka 200 kwa gharama ya tsh milioni mbili (2,000,000 tsh) 
2. Kofia kubwa (kwa ajili ya jua) na tshirts 200 kwa gharama ya milioni moja na laki sita (1,600,000 tsh) 
3. Vyandarua 100 kwa gharama ya laki nane (800,000 tsh) 
4.Sweta 200 kwa gharama ya milioni moja laki sita na tisini na saba (1,697,000 tsh) 
Tunaomba wadau wote na watanzania kwa ujumla kwenye jumuiya yetu tuendelee kuwa mstari wa mbele katika kusaidia misaada mbalimbali katika jamii mbalimbali zenye mahitaji huko Tanzania. 
TCO itaendelea kuwa mstari wa mbele kila mwaka kuendeleza zoezi hiliKwa pamoja tutainuana. 
Karibu na changia kwa bidii tarehe 10 Dec 2016 Oakland- California kwenye hii. 
Tembelea website yetu 
Erick Byorwango 
(Mwenyekiti- Uhusiano na Uenezi TCO)





Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...