Na Humphrey Shao,Globu ya Jamii

Chama cha wafanyakazi wa migodini na kazi za ujenzi (TAMICO), kimewataka wadau na wafanyakazi ambao wanafanya kazi katika mashirika ya ujenzi kujiunga na chama hicho.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam mwenyekiti wa TAMICO Taifa,Mhandisi Fred Kapamila,amesema kuwa matokeo ya huru na utandawazi ni ajira isiyo na staha kwasababu makampuni yanawania kupata faida zaidi kupitia kuwapunja wafanyakazi wao.

"Tarehe 18/10/2016 chama kilifanya mkutano wake mkuu na kupata safu ya viongozi wapya hivyo uongozi mpya unawaomba watu wenaofanya kazi katika makampuni ya migodi kujiunga kwa wingi katika chama hicho hili waweze kupata msaada pindi wanapopata matatizo"amesema Kapilima.

Amesema kuwa uongozi mpya umejitayarisha vya kutosha kupambana na changamoto za kuhakikisha dhamira na matarajio ya wanachama yanafikiwa katika kipindi kijacho cha  miaka mitano.

Alitoa wito kwa serikali kuangalia upya maslahi ya wafanyakazi wa migodini ambao wamekuwa wakiteseka kila kukicha.
Mwenyekiti wa wa chama cha wafanyakazi  wa Migodi,Nishati,ujenzi na kazi nyinginezo nchini,TAMICO,Mhandisi Fred Kapimila,akizungumza na Waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam,kulia kwake ni katibu wa chama hicho,  Thomas Sabai,kushoto  Afisa elimu na mafunzo Philotea Ruvumbagu,

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...