Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Tanzania, (TANESCO), Felchesmi Mramba, (kushoto), akibadilishana hati za mkabata na Mkurugenzi wa Maendeleo ya Biashara ya Kimataifa wa kampuni ya Bouygues Energies&Service, Patrick Canton baada ya kusini, mradi wa ujenzi wa njia ya umeme (transmission line) itakayounganisha Tanzania na Kenya, makao makuu ya TANESCO jijini Dar es Salaam, Oktoba 7, 2016. Shirika hilo limeingia mkataba na makampuni matatu kutekeleza mradi huo (KTPIP), wa Msongo wa KV400 unaofadhiliwa na Benki ya Maendeleo ya Afrika, (AfDB) na Shirika la Misaada ya Maendeleo la Japan, (JICA), kwa gharama ya dola za Kimarekani
309.26
NA
K-VIS MEDIA/Khalfan Said.
SHIRIKA
la Umeme nchini Tanzania, (TANESCO), limesaini mkataba na makampuni matatu
kujenga njia ya umeme, (Transmission lines), wa Msongo wa Kilovolti 400 utakaounganisha
Tanzania na Kenya.
Hafla
ya kutiliana saini mikataba hiyo, imefanyika leo Oktoba 7, 2016 makao makuu ya TANESCO
jijini Dar es Salaam, ambapo Shirika hilo la Umeme linalomilikiwa na serikali,
limetiliana saini mikataba hiyo na makampuni ya Bouygues Energies Service,
Energoinvest na Kalpa-Taru.
Akizungumz
wakati wa hafla hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Mhandisi, Felchesmi
Mramba, alisema, Ujenzi wa Mradi huu wenye urefu wa Kilomita 414, utaanzia
Mkoani Singida,-Babati-Arusha hadi Namanga kwenye mpaka wa Tanzania na Kenya.
Kisha
Mradi utaunganishwa na njia ya Msongo wa Kilovolti 400 yenye urefu wa kilomita
96 kutoka eneo la Isinya, Nairobi, nchini Kenya hadi eneo la mpaka wa Tanzania
na Kenya, (Namanga) ambapo utaunganisha na njia ya umeme wa wa Msongo wa
Kilovolti 400kv kwa upande wa Tanzania.
“
Napana niwahakikishie, kuwa huu ni mfululizo wa miradi mikubwa inayotekelezwa
na TANESCO na utawezesha usafirishaji wa umeme wa Mgawati 2000 katika pande
zotekenya na Tanzania”. Alifafanua Mramba.
Akifafanua
zaidi, Mhandisi Mramba alsiema, utekelezaji wa mradi huu unaofadhiliwa na Benki
ya Maendeleo ya Afrika, (AfDB), na Shirika la Misaada ya Maendeleo la Japan,
(JICA), kwa gharama ya Dola za Kimarekani, Milioni 309.26 utakamilika katika
kipindi cha miezi 24, sawa na miaka 2.
Kusoma zaidi bofya HAPA.
Kusoma zaidi bofya HAPA.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...