Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo ( wa nne kutoka kulia) katika picha ya pamoja na wawakilishi kutoka Benki ya Maendeleo  ya  Afrika (AfDB), Ubalozi wa  Sweden na Shirika la Maendeleo  la  Umoja wa Mataifa (UNDP).
 

Tanzania inatarajiwa kuwa mwenyeji wa Kongamano litakalokutanisha nchi mbalimbali za Afrika kwa ajili ya kujadili na kubadilishana uzoefu katika masuala ya Nishati linalotarajiwa kufanyika Aprili mwaka 2017. Hayo yameelezwa na Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo alipofanya kikao na wawakilishi kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Kampuni ya Uendelezaji wa Jotoardhi Tanzania (TGDC) Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), Ubalozi wa Sweden na Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP).
 Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (kushoto) akiongoza kikao kilichokutanisha wawakilishi kutoka kutoka Wizara ya Nishati na Madini,  Benki ya Maendeleo  ya  Afrika (AfDB), Ubalozi wa  Sweden na Shirika la Maendeleo  la  Umoja wa Mataifa (UNDP). Kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa  Nishati na Madini anayeshughulikia Madini, Profesa James Mdoe.
 Wawakilishi kutoka Benki ya Maendeleo  ya  Afrika (AfDB), Ubalozi wa  Sweden na Shirika la Maendeleo  la  Umoja wa Mataifa (UNDP), wakifuatilia maelezo  yaliyokuwa yanatolewa na  Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (hayupo pichani) katika kikao hicho.
 Wawakilishi kutoka Wizara ya Nishati na Madini na Kampuni ya Uendelezaji wa Jotoardhi Tanzania (TGDC) wakifuatilia maelezo yaliyokuwa yanatolewa na Mkurugenzi Mkazi wa na Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Awa Dabo (hayupo pichani) katika kikao hicho.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...