Mpendwa wetu Fatuma  Salum (pichani, enzi za uhai wake) akiwa huko Mozambiki katika kutafuta maisha, ametutoka Duniani akiwa katika maandalizi ya kurudi nyumbani kwao kuiona familia yake na Mzazi wake na ndugu zake waishio Kinondoni maeneo ya Mkwajuni  Jijini Dar es Salaam.
Siku mbili nyuma Marehemu Fatma aliugua ugonjwa wa kuishiwa nguvu mkono na mguu upande mmoja na kukimbizwa Hospitali ambako alipata bahati ya kuongea na mama yake Mzazi na kumweleza hali yake. 
Baada ya hapo tulipata taarifa ya kuwa amefariki akiwa katika maandalizi ambapo Ijumaa hii iliyopita alitarajia  aanze safari, na Ijumaa hiyo hiyo mchana akaaga Dunia.

Hadi sasa wafanya biashara wenzake kwa kushirikiana na familia ya mpendwa wetu mwili utalala Boda na asubuhi safari itaanza.
Familia ya mpendwa wetu inatoa asante kwa wote walioshiriki kufanikisha michango yao na kujinyima ili kufanikisha safari ya mpendwa kurudishwa nyumbani na wote wanao endelea kutoa misaada ya hali na mali. Shukrani za kipekee ziwafikie wafanya biasha wenzake pamoja na Madaktari wote na ndugu na jamaa kwa kufanikisha taratibu za maandalizi ya safari yake ya mwisho
Inna lillahi wa inna ilayhi raji'un 
إِنَّا لِلّهِ وَإِنَّـا إِلَيْهِ رَاجِعون

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...