Arusha Press Club inawataarifu kuwa inasikitika kutangaza kifo cha Mama yake mzazi wa bndugu yetu ambaye alikuwa mwenyekiti wa kwanza wa Arusha press club Nicodemus Ikonko (pichani akiwa na marehemu) na ambaye kwa sasa ni Mhariri Mkuu wa gazeti la Serikali la Habari Leo jijini Dar es salaam.
Mama amefariki jana saa tatu asubuhi akiwa anapata matibabu katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Kuhusu taratibu za maziko tutaendelea kujuzana hapo baadae. Mipango ya mazishi yanafanyika nyumbani kwa Bw. Ikonko huko Ukonga jijini Dar es salaam.
Habari zaidi tutazitoa kadri zitapotufikia.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...