Na Theresia Mwami TEMESA Shinyanga

Wakala wa Ufundi na Umeme TEMESA Mkoa wa Shinyanga inazidai Halamashauri, Mashirika na Taasisi za Serikali mkoani humo jumla ya shillingi 163,269,269.82 kutokana na kupata huduma ya matengenezo ya magari.

Katika taarifa yake kwa Mtendaji Mkuu wa TEMESA, Meneja wa TEMESA Shinyanga Mhandisi Riziki Lukali amesema madeni hayo ni ya mwaka wa fedha 2016/2017 na wamesha wasilisha madai yao kwa wahusika na wanasubiri kulipwa.

Mhandisi Riziki Lukali aliwataja wadaiwa hao kuwa ni TANROADS Shinyanga Sh 24,193,733.21, TANESCO Shinyanga Sh Milioni 96,267,987.63, DED Kishapu Sh 6,753,735.03, RAS Shinyanga Sh 2,742,097.36, KUWASA Kahama Sh 9,855,714, KASHUWASA Shinyanga Sh 1,992,430, TBA Shinyanga Sh 5,103,062.56, Mahakama Kuu Shinyanga Sh 5,470,628.91, Uhamiaji Shinyanga Sh 896,333.63, DAS Kishapu Sh 1,071,573.57, NSSF Shinyanga Sh3,798,184 pamoja na RMO Shinyanga shilingi 5,123, 789.92 milioni na jumla ya madeni hayo yote ni Sh 163,269,269.82.

Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme TEMESA Dkt. Mussa Mgwatu amefurahishwa na utaratibu wa TEMESA Shinyanga wa kuzuia magari ya taasisi, halmashauri na mashirika yanayodaiwa na kituo hadi hapo yatakapolipiwa gharama za matengenezo.
Mtendaji Mkuu TEMESA Dkt. Mussa Mgwatu (wa pili kulia) akitoa maelekezo kwa watendaji wa kituo cha Shinyanga alipotembelea kituoni hapo katika ziara yake katika vituo vya TEMESA Kanda ya Ziwa.
Mtendaji Mkuu TEMESA Dkt. Mussa Mgwatu (menye shati la rangi ya bluu)akiangalia gari la TANESCO Shinyanga, linaloshikiliwa na TEMESA Shinyanga kwa sababu ya deni la Sh Millioni 96 kushoto ni Meneja wa TEMESA Shinyanga Mhandisi Riziki Lukali.Picha zote na Theresia Mwami TEMESA Shinyanga.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...