Na Luteni Selemani Semunyu JWTZ

Mchezaji wa Klabu ya Golf ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania ya Lugalo Nicholous Chitanda imeibuka washindi wa Jumla katika mashindano ya wazi ya PWC Trophy yaliyofanyika Jumamosi Oktoba 22 katika uwanja wa Golf wa Lugalo Jijini Dar es Salaam.

Chitanda aliibuka na ushindi huo nakuwashinda wachezaji wengine zaidi ya 100 waliojitokeza kutoka Klabu zote Nchini baada ya kupata Mikwaju au Gross 74 huku kiwango chake cha Uchezaji kikiwa ni Tisa na hivyo kuibuka na Mikwaju ya Jumla Net ya 65.

Katika Division A ushindi ulinyakuliwa na Isack wanyenche kutoka Klabu ya Arusha baada kupiga mikwaju 69 huku kiwango chake cha uchezaji kikiwa ni Tatu na hivyo kuibuka na ushindi kwa kupiga mikwaju ya jumla 66 na kufuatiwa na Juma Likuli wa Lugalo baada ya kupiga mikwaju ya jumla 68.
Kwa upande wa Division B mshindi ni Dk James Legg wa Lugalo baada ya kupiga mikwaju 84 huku kiwango chake cha uchezaji kikiwa ni 13 na hivyo kuwa na mikwaju ya jumla 71 na kufuatiwa na Salum Mvita wa Dar es Salaam Gymkhana kwa mikwaju ya Jumla 71.

Division C kwa upande wake Mpiga Golf Reneir Kuhcmanu wa Lugalo aliibuka na ushindi katika kundi hilo baada ya kupiga Mikwaju ya Jumla 68 huku kiwango chake cha uchezaji kikiwa ni 24 akifuatiwa na Kapten Amanzi Mandengule wa Lugalo pia baada ya kupata mikwaju ya Jumla 69 huku kiwango chake cha uchezaji kikiwa ni 19..
Mshindi wa Jumla wa mashindano ya PWC yaliyofanyika Jumamosi Oktoba 22 Jijini Dar es Salaam Nicholous Chitanda wa Lugalo aliyeshika Vikombe akiwa katika Picha ya pamoja mara baada ya kukabidhiwa Kushoto ni mwenyekiti wa Klabu ya Lugalo Brigedia Jenerali Michael Luwongo , wa kwanza kulia ni Mwenyekiti wa TGU Joseph Tango na wa pili kulia ni Msuya Mkurugenzi PWC .(Picha na Luteni Selemani Semunyu).

Wachezaji wa Golf kutoka kushoto ni Katibu Mkuu Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mh Job Masima, Dk Edmund Mndolwa aliyekuwa Mkuu wa majeshi Jenerali Mstaafu George Waitara na Balozi Clemence Sanga wakibadilshana mawazo kabla ya kuanza mashindando ya PWC yaliyofanyika Jumamosi Oktoba 22 katika Uwanja wa Golf Lugalo Jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...