Katika kusaidia kuboresha elimu nchini, Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) limesaini mikataba miwili na serikali kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia iliyo na lengo la kusaidia elimu nchini.

Mkataba wa kwanza unahusu mradi unaofahamika kama 'Empowering Adolescent Girls and Young Woman through Education' mradi ambao umedhaminiwa na Shirika la Misaada la Korea (KOICA) kwa kiasi cha pesa cha Dola Milioni tano (5,000,000), mradi ambao unataraji kufanyika katika wilaya ya Ngorongoro, Sengerema, Kasulu na Micheweni, Pemba.

Mkataba wa pili unahusu mradi wa 'XPRIZE - Promotion of Early Learning Through the use of Innovative Technologies' ambao umedhaminiwa na UNESCO kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula (WFP) kwa kiasi cha pesa cha Dola Milioni mbili (2,000,000) ambapo utahusisha watu wa miaka 15-18 ambao hawapo shuleni kutoka Arusha na Tanga ambapo watapatiwa tablet ambazo zitakuwa na programu tumishi za kujifunza.

Akizungumza wakati wa kusaini mikataba hiyo, Mkuu wa ofisi na Mwakilishi wa UNESCO, Zulmira Rodrigues alisema mipango ya UNESCO ni kuona inawasaidia watoto ambao hawasomi licha ya kuwa na umri wa kuwa shuleni wakipata nafasi ya kusoma ili kupunguza idadi ya watoto ambao hawapo shuleni duniani ambapo takwimu zinaonyesha wanazidi Milioni 263.
Mkuu wa ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues akizungumza kuhusu mradi wa Empowering Adolescent Girls and Young Woman through Education na XPRIZE - Promotion of Early Learning Through the use of Innovative Technologies.

"Tunaandika histori leo sio kwa Tanzania bali dunia nzima, maana makubaliano yataleta ushirikiano kati ya WFP, UNESCO na Wizara ya Elimu kuwasaidia watoto zaidi ya Milioni 263 ambao hawapo shuleni duniani na kutumia nafasi ya teknolojia kutafuta suluhisho la kuwasaidia watoto hawa,

"Tunaishukuru Wizara ya Elimu kwa kutuamini, nawashukuru WFP kwa kuwa pamoja nasi na kwa washirika wengine ambao wamekubali kuungana nasi kwa ajili ya kufanikisha hili," alisema Rodrigues.

Nae Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Maimuna Tarish alisema msaada huo utaweza kusaidia kuboresha elimu nchini hasa katika kipindi hiki ambacho serikali inajipanga kutoa elimu kisasa kwa kutumia njia za kidigitali na hivyo ni mwanzo mzuri kwa mfumo ambao wanajipanga kuanza kuutumia.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Maimuna Tarish akitoa neno la shukrani kwa niaba ya serikali.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...