MFUKO  wa Uwekezaji wa Pamoja  (UTT-AMIS)  umesema  kutokana na utafiti walioufanya  kwa muda wa miaka 10, unaonyesha Watanzania walio wengi  hawana  uelewa  wa   kuwekeza fedha zao  kwenye hati fungani (bond).
 Kauli hiyo  imetolewa  jijini Dar es Salaam na  Mkurugenzi wa Masoko na Uhusiano wa  UTT,  Daudi Mmbaga , alisema  watu wengi wanakuwa na fedha nyingi lakini hawajui  jinsi ya kuwekeza  fedha zao.
 Alisema  kutokana na  changamoto iliyopo kwa Watanzania  ya kutokuwa na uelewa wa  jinsi ya kuwekeza , wameamua kuanzisha huduma ya  Usimamizi wa Mali  itakayomsaidia mwananchi  jinsi ya kuweza kuwekeza fedha zake na kutengeneza faida.
“ Watu wengi   wanakuwa  na fedha nyingi  lakini  zimelala tu, na wengine  wamewekeza   kwenye maeneo yasiyowapa faida  ndio maana tuamua kuanzisha huduma itakayowasaidia  kuwekeza  fedha yao  inayoitwa  Usimamizi wa Mali,” alisema.
 Aidha, alisema huduma hiyo  kwa sasa imeshaanza kutumika na  mwelekeo   ni mzuri  kutokana na  watu wengi  kupenda kuwekeza fedha zao, ambapo kiwango cha kuanzia ni sh. Milioni  tano.
 Mmbaga  alisema   kiwango  cha elimu  nchini  kikijikita vizuri kitasababisha  kuwepo  na soko la uhakika   na kusababisha  kuwepo na maendeleo   ya kiuchumi.
 Hata hivyo  aliwashauri wananchi kujitahidi kuwekeza katika mifuko  ya uwekezaji  kwa kuwa  kutasaidia  kuwa na imani na fedha zao.
Mkurugenzi wa Masoko na Uhusiano wa Mfuko wa Uwezeshaji (UTT-AMIS), Daud Mbaga akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, kuhusu huduma yao mpya ya usimamizi wa mali. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji, Issa Wahichinenda. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...