Na: Genofeva Matemu – WHUSM

Vijana nchini wametakiwa kujitokeza kwa wingi kupima afya zao ili waweze kujitambua na kupata mbinu mbadala zitakazowazesha kujikinga na maambukizi ya virusi vya ukimwi ili kujenga taifa lililo na afya bora.

Hayo yamesemwa na Mwezeshaji kutoka Baraza la Taifa la Watu Wanaoishi na Virusi vya Ukimwi (NACOPHA) Bw. Hamidu Mkwinda alipokua akizungumza na vijana waliojitokeza kupata elimu ya namna ya kujikinga na maambukizi ya virusi vya ukimwi wakati wa wiki ya vijana kitaifa na kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru leo katika Viwanja vya Sabasaba Mkoani Simiyu.

“Vijana wanatakiwa kujitambua na kujua haki zao ili wasije wakaangukia katika wimbi la ulaghai na anasa ambazo zitawapelekea kutokufikia malengo yao na wakati mwingine kupata maambukizi ya virusi vya ukimwi bila kutarajia” amesema Bw. Mkwinda.

Aidha Bibi. Happiness Malamala kutoka NACOPHA amewataka vijana kutokukata tamaa pale wanapojitambua kuwa wamepata maambukizi ya virusi vya ukimwi kwani kuwa na virusi vya ukimwi sio mwisho wa maisha bali watambue kwamba virusi vya ukimwi ni kama magonjwa mengine yasiyotibika kama vile kisukari, kansa na presha.
Mratibu kutoka Baraza la Taifa la Watu Wanaoishi na Virusi vya Ukimwi (NACOPHA) Bw. Joseph Muhoja (kulia) akizungumza na vijana wenye umri chini ya miaka 18 kuhusu namna kijana anavyopaswa kujitambua na maambukizi ya virusi vya ukimwi leo katika viwanja vya Sabasaba kuelekea kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu.
Baadhi ya vijana wenye umri chini ya miaka 18 wakifuatilia mada iliyokua ikitolewa na Baraza la Taifa la Watu Wanaoishi na Virusi vya Ukimwi leo katika viwanja vya Sabasaba kuelekea kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu.
Mjumbe kutoka Baraza la Taifa la Watu Wanaoishi na Virusi vya Ukimwi Bibi. Happiness Malamala (kulia) akitoa elimu ya namna ya kutumia kinga kuzuia maambukizi ya virusi vya ukimwi kwa vijana waliotembelea banda la NACOPHA leo katika viwanja vya Sabasaba kuelekea kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...