Katika kukabiliana na upungufu wa ajira hapa nchini Vijana wameshauriwa kujiajiri kupitia Sanaa na vipaji walivonavyo katika kupata kipato.
Ushauri huo umetolewa Wilayani Bagamoyo na Kaimu Mkurugenzi Idara ya Maendeleo ya Sanaa kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bibi Leah Kihimbi alipokuwa anawahutubia wahitimu wa Astashahada na Stashahada ya Sanaa na Ufundi katika Chuo cha Sanaa na Ufundi Bagamoyo kilichopo chini ya Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa).
“Tumieni elimu mliyopata kujiajiri wenyewe ili kuepuka changamoto ya ajira iliyopo hapa nchini, ujuzi mliopata ni njia pekee ya kujiletea kipato na Taifa kwa ujumla”.Alisema Bibi Leah.
Aidha Kaimu Mkurugenzi huyo aliongeza kuwa wasanii wote wanaofanya kazi za Sanaa ni vyema wakasajili kazi zao katika Mamlaka husika ili iwe rahisi kwa Serikali kutoa msaada kwa urahisi kwaWasanii hao.
Kwa upande wake Mtendaji Mkuu waTaasisi ya Sanaa na Utmaduni Bagamoyo (TaSUBa) Dkt.Herbet Makoye aliwasihi wahitimu hao kuwa mabalozi wazuri wa sanaa watakapokuwa wanafanya shughuli zao za Sanaa.
“Nendeni mkawe mabalozi wazuri wa Chuo chetu kwa kuwa Wasanii bora na kutengeneza kazi nzuri ili muweze kushindana na soko la ajira”. Alisisitiza Dkt.Makoye.
Naye mhitimu wa ngazi ya Stashahada ya Sanaa na Ufundi Bi Imelda John amesema kuwa elimu aliyoipata itamsaidia kufanya kazi ya Sanaa kwa weledi zaidi hasa katika fani ya kutengeneza Filamu na Picha Jongefu.
Mahafali hayo ni ya 27 katika chuo hicho ambapo kwa mwaka huu jumla ya wanafunzi 85 wametimu Astashahada na Stashahada ya Sanaa na Ufundi. imeandikwa na Shamimu Nyaki- WHUSM.
aimu Mkurugenzi Idara ya Maendeleo ya Sanaa kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bibi Leah Kihimbi akizungumza na wahitimu pamoja na wageni mbalimbali (hawapo pichani) katika sherehe za mahafali ya 27 ya Chuo cha Ufundi na Sanaa Bagamoyo kilichopo chini ya Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) Oktoba mosi Wilayani Bagamoyo.
Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo Dkt.Herbet Makoye akisoma hotuba kwa Mgeni Rasmi pamoja na wageni mbalimbali (hawapo pichani) katika sherehe za mahafali ya 27 ya Chuo cha Ufundi na Sanaa Bagamoyo kilichopo chini ya Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) Oktoba mosi Wilayani Bagamoyo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...