kig3
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Bara, Mhe. Phillip Mangula akiwasilisha mada kuhusu Maadili ya Viongozi wakati wa Kongamano la Maadhimisho ya Kumbukizi za Mwalimu Julius Nyerere lililofanyika jana Jijini Dar es Salaam katika ukumbi wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere(MNMA). Maadhimisho hayo yamefanyika ikiwa ni kumbukumbu za miaka 17 tangu Baba wa Taifa Mwl. Nyerere afariki dunia.
kig1
Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Mhandisi Stella Manyanya akimpongeza Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Bara, Mhe. Phillip Mangula mara baada ya kuwasilisha mada kuhusu Maadili ya Viongozi wakati wa Kongamano la Maadhimisho ya Kumbukizi za Mwalimu Julius Nyerere lililofanyika jana Jijini Dar es Salaam katika ukumbi wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere(MNMA).Kutoka kushoto ni Mkuu wa Chuo hicho Profesa Shadrack Mwakalila, Mwenyekiti wa Kongamano hilo ambaye pia ni Spika wa Bunge la Jamhuri msaafu Mhe. Anne Makinda.
kig5
Baadhi ya washiriki wa Kongamano la Maadhimisho ya Kumbukizi za Mwalimu Julius Nyerere wakifuatilia mada kutoka kwa wawasilishaji ambao ni Mhe. Phillip Mangula, Joseph Butiku, Ibrahim Kaduma na Dkt. Harun Kondo, mada zilizowasilisha ni pamoja na Miiko ya Uongozi, Azimio la Arusha na Maadili ya Viongozi.
kig7
Mchumi Mwandamizi Profesa Ibrahim Lipumba akichangia mada wakati wa Kongamano la Maadhimisho ya Kumbukizi za Mwalimu Julius Nyerere lililofanyika jana Jijini Dar es Salaam katika ukumbi wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere(MNMA). Maadhimisho hayo yamefanyika ikiwa ni kumbukumbu za miaka 17 tangu Baba wa Taifa Mwl. Nyerere afariki dunia.
kig13
Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia alikuwa Mwenyekiti wa Kongamano la Maadhimisho ya Kumbukizi za Mwalimu Julius Nyerere lililofanyika jana Jijini Dar es Salaam katika ukumbi wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere(MNMA) akiagana na washiriki.Picha na. Frank Shija, MAELEZO.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...