Afisa Mkuu wa Idara ya huduma kwa wateja wa Vodacom Tanzania,Harriet Lwakatare akiongea na baadhi ya wateja waliofika kupata huduma mbalimbali katika duka la kampuni hiyo lililopo Mlimani city jijini Dar es Salaam leo ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha wiki ya huduma kwa wateja duniani.
Baadhi ya wateja wa Vodacom Tanzania waliofika kupata huduma mbalimbali katika duka la kampuni hiyo lililopo Mlimani city jijini Dar es Salaam leo wakichukua keki kutoka kwa Afisa Mkuu wa Idara ya huduma kwa wateja wa Vodacom Tanzania,Harriet Lwakatare(kushoto) ikiwa ni sehemu ya kufurahia kwa pamoja kuadhimisha wiki ya huduma kwa wateja duniani.
Mmoja wa wateja wa Vodacom Tanzania aliyefika kupata huduma mbalimbali katika duka la kampuni hiyo lililopo Mlimani city jijini Dar es Salaam leo akifurahi jambo wakati alipokuwa akipewa keki na Afisa Mkuu wa Idara ya huduma kwa wateja wa kampuni hiyo,Harriet Lwakatare(kulia) ikiwa ni sehemu ya kufurahia kwa pamoja kuadhimisha wiki ya huduma kwa wateja duniani.
Baadhi ya maafisa waandamizi wa Vodacom
Tanzania,wakiwa wamebeba keki tayari kwa kuwagawia wateja na wafanyakazi wa kampuni hiyo ikiwa ni
sehemu ya kufurahia kwa pamoja kuadhimisha wiki ya huduma kwa wateja duniani.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...