WAKAZI wa jiji la Dar es Salaam washauriwa kuchangamkia fursa ya zoezi la Unywaji dawa za magonjwa ambayo yalikuwa hayapewi kipaumbele kwa jamii ili waweze kujikinga na magonjwa hayo.  

Magonjwa hayo ni pamoja Mabusha, matende, usubi, Minyoo zitakazo kuwa zinatolewa katika vituo vya afya vyote vya mkoa pamoja na kwenye mikusanyiko ya watu.

Akizungumza leo katika uzinduzi wa zoezi hilo la unywaji wa dawa hizo litakalochukua siku tano kwa mganga mkuu wa mkoa Grace Magembe amesema wagonjwa watakaopatikana na tatizo hilo la watafanyiwa upasuaji.

“Tumeandaa vituo vya afya pugu, na Mbweni mission ambako upasuaji utakuwa unaendelea huku tukishirikiana na madaktari kutoka hospitali ya Muhimbili.”

Ameongeza kuwa mpaka sasa zoezi la upasuaji litaendelea hadi mwezi wa 12 mwaka huu, ambapo mpaka hivi sasa zaidi ya wagonjwa 104 wameshafanyiwa upasuaji.

“Zoezi hili tumelipa sana kipaumbele ili kuokoa nguvu kazi ya taifa, tumeandaa vituo zaidi ya 281 kwa ajili ya zoezi  hili wanaume kwa wanawake wajitokeze kumeza dawa hizi”.

Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda amewataka wananchi kuepuka maneno yayozungumzwa mitaani kuwa dawa zinamadhara hivo kujitokeza kumeza dawa ili waepukanae na magonjwa hayo.

“Zoezi linaendelea vyema watanzania wajitokeze, pia na zoezi la usafi liendelee ili kuepuka mazalia ya mbu ambao ni vigumu kuwatambua wanaeneza ugonjwa huu’’.

Wizara ya afya na ustawi wa jamii inaendesha zoezi hili kuanzia mwaka 2009, huku kwa mkoa wa Dar es saam wakitarajiwa kuwafikiwa wananchi zaidi ya milioni 4 , ili kuwakinga na magonjwa hayo.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam akiongea na wananchi kujitokeza katika zoezi la unywaji wa dawa leo jijini Dar es salaam.
Mganga mkuu wa Mkoa Grace Magembe akihimiza wananchi kuhusu kujitokeza kupata chanjo ya Mabusha na Matende jijini Leo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...