Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii .

MAMLAKA ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (Tantrade) imeanzisha mafunzo ya Ushonaji Nguoa kwa watu wasioona ambayo yatatolewa kwa miezi mitatu kuendeshwa na fundi mahiri wa nguo za kushona, Abdallah Nyangalio.

Akizungumza na katika uzinduzi wa mafunzo hayo, Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Felix Lyaniva amesema kuwa mafunzo hayo yatasaidia watu wasioona kuweza kujiajiri na kuongeza kipato cha kuacha kuombaomba.

Amesema kuwa mwanafunzi mmoja ambaye atafanya vizuri katika mtihani wa mafunzo hayo atatoa cherehani ikiwa ni pamoja na mwanafunzi mmoja wa Temeke kwa kila mzunguko atatoa cherehani moja.

Nae Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka hiyo, Edwin Rutageruka amesema kuwa kuendesha mafunzo hayo ni kutaka watu wasioona waweze kujikwamua kiuchumi kwa kuwapa mafunzo ya ushonaji nguo.

Rutageruka amesema kuwa Mamlaka imeona kendesha mafunzo katika wilaya tano kwa kuanzia kwa Manispaa ya Temeke kwa kila Darasa litakuwa na watu saba.Mkufunzi wa mafunzo hayo, Abdallah Nyangalio amesema kuwa watu wenye ulemavu wanaweza kufanya kila kitu na kuwa hivyo sio kigezo cha kufanya kuombaomba.
Mkuu wa Wilaya Temeke Mh.Felix Lyaniva (kulia) akimkabidhi zawadi ya Cherehani Mkufunzi wa Mafunzo wa ushonaji kwa wasioona Bw. Abdallah Nyangalio wakati wa uzinduzi wa mafunzo hayo jijini Dar es Salaam,wa kwanza kusoto ni Bw. Edwin Rutageruka Kaimu Mkurugenzi Mkuu Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (Picha na Benjamin Sawe Maelezo).
Mkuu wa Wilaya Temeke Mh.Felix Lyaniva (kulia) akiongea na Mkufunzi wa Mafunzo wa ushonaji kwa wasioona Bw. Abdallah Nyangalio wakati wa uzinduzi wa mafunzo hayo jijini Dar es Salaam ambapo Mkuu wa wilaya hiyo amewaasa watu wenye ulemavu kutokata tamaa kimaisha kwani jambo lolote ukiwa na nia nalo na kulifanya kwa nidhamu na kujituma utafanikiwa(Picha na Benjamin Sawe Maelezo).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...