Na Humphrey Shayo -Globu ya Jamii.
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Ally Hapi, ametoa wito kwa wakazi wa Kinondoni na Tanzania kwa ujumla kumuenzi Mwalimu Nyerere kwa kufanya shughuli zenye manufaa kwa jamii inayotuzunguka.
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Ally Hapi, ametoa wito kwa wakazi wa Kinondoni na Tanzania kwa ujumla kumuenzi Mwalimu Nyerere kwa kufanya shughuli zenye manufaa kwa jamii inayotuzunguka.
Hapi ameyasema hayo leo, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika fukwe za Coco beach Dar es Salaam wakati wa zoezi la kufanya usafi katika fukwe hizo,ikiwa ni sehemu ya ishara ya kumuenzi Mwalimu kwa urithi aliotuachia.
"Hii ni moja ya sehemu ambazo tunapasa kujivunia, kwani mwalimu aliamua kutenga maeneo haya kwa watu wa hali ya chini kuja kujiburudisha tena pasipo kulipia chochote, hivyo kamwe matajiri hawatopata fursa ya kuja kujipenyeza katika kunyakua eneo hili ambalo kila Mtanzania anakuja kujidai nalo" amesema Hapi.
Alimaliza kwa kusema kuwa usafi ni jambo la msingi na linapaswa kufanywa kila siku,tusingojee mahadhimisho au sikukuu,pia alichukua fursa hiyo kuwashukuru wakazi wa Kinondoni kwa kujitokeza kwa wingi katika zoezi hilo.
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni,Ally Hapi, akisukuma mkokoteni wenye taka.
Baadhi ya Wanafunzi wakiwa na walimu wao katika zoezi la usafi lililofanyika CocoBeach Dar es Salaam.
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Ally Hapi, akimwaga takataka kwa kutumia toroli wakati wa zoezi la usafi kitika fukwe za Coco Beach.
Mkuuwa wilaya ya Kinondoni Ally Hapi akiweka taka kwenye mfuko ulioshikwa na Mkandarasi wa fukwe za Kinondoni Elizabeth Mhlanga kutoka kampuni ya Flamingo,wakati wa zoezi la usafi katika fukwe za Coco Beach.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...