Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii

Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, imesema kulinda viwanda vya ndani ni lazima watanzania wanunue bidhaa zinazozalishwa ndani na kuacha bidhaa zinazozalishwa nje ya nchi.

Hayo ameyasema leo, Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage, wakati akitangaza maonesho ya viwanda vya ndani yatakayofanyika Desemba 7 hadi 11 katika viwanja vya sabasaba jijini Dar es Salaam.

Mwijage amesema nchi zilizofanikiwa kwa viwanda imetokana na watu wao kupenda kununua bidhaa zao ambapo na Tanzania inatakiwa kufanya hivyo kwa wananchi kupenda bidhaa zao

Amesema viwanda vya ndani katika kuweza kuzalisha bidhaa na zikaweza kutoka ni lazima wazalishe bidhaa zenye ubora kwa kupata soko la ndani na nje ya nchi. ‘’Kauli mbiu ya maonesho hayo ni Tanzania sasa tunajenga viwanda ambapo kila mtu anaweza kuanzisha kiwanda chake na kuzalisha na kuweza kupata soko la uhakika’’.

Amesema maonesho hayo yatakutanisha wadau mbalimbali wa viwanda ambapo watanzania wenye nia kuanzisha viwanda watumie maonesho hayo kuweza kupata mwongozo kutoka kwa wataalam jinsi ya kuanzisha kiwanda. Aidha amesema katika maonesho hayo kwa wanafunzi waliohitimu katika vyuo watumie fursa katika ya kutafuta ajira kwa viwanda vitavyoshiriki maonesho hayo.

Amesema Wakuu wa Mikoa wote wataalikwa kuweka maeneo yao waliopanga kwa ajili ya uwekezaji wa viwanda ikiwa ni pamoja kuondoa masharti magumu kwa wawekezaji wanakwenda kuomba ardhi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...