Na Hussein Makame, NEC
Watanzania wengi hawaijui Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), majukumu yake na miongozo inayoongoza uchaguzi, hali inayosababisha manung’uniko mengi na upotoshaji kwa umma juu ya tume hiyo.
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Bw. Kailima Ramadhani (pichani) wakati akitoa tathmini ya elimu ya mpiga iliyotolewa hivi karibuni kwenye Mkutano Mkuu wa 32 wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT) uliofanyika wiki mbili zilizopita mjini Musoma.
Bw. Kailima alisema kutokana na hali hiyo, NEC imeanza kutekeleza mkakati kabambe wa kutoa elimu ya mpiga kura kupitia njia mbalimbali ikiwemo kushiriki kwenye maonesho na mikutano inayojumuisha wadau muhimu wa uchaguzi. Taarifa kamili BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...