Timu ya soka ya Watumishi FC wilayani Kishapu Mkoa wa Shinyanga imenyakua ubingwa wa michuano ya Mwenge wa Uhuru kuwania Kombe la Ng’ombe.
Katika michuano hiyo iliyotimua vumbi jana jioni, timu hiyo inayoundwa na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu iliibamiza kwa mikwaju ya penati Igaga FC mabao 4-2.
Mchezo huo uliochagizwa na hamasa kutoka kwa mashabiki ukichezwa uwanja wa shule ya msingi Mhunze, ulimalizika kwa dakika 90 huku ubao wa matokeo ukisomeka 1-1 yaliyofanya mikwaju ya penati zipigwe.
Katika matokeo ya mikwaju ya penati timu hiyo ya watumishi iliibuka kidedea na inatarajiwa kukabidhiwa zawadi yao ya ng’ombe Ijumaa katika kilele cha Mwenge wa Uhuru wilayani humo.
Awali kabla ya mchezo wa fainali kulikuwa na mechi kati ya Talents FC na Bodaboda zote za mjini Mhunze wilayani humo kutafuta mshindi wa tatu.
Hadi refa anapuliza kipyenga cha mwisho Talents walikuwa wameondoka na ushindi wa bao 1-0 na kuibuka washindi wa tatu.
Michuano ya kuwania kombe la ng’ombe ilianza wiki mbili zilizopita wilayani humo ikiwa na lengo la kuwajengea vijana ari ya kujituma na kujiletea maendeleo.
Mkuu wa Wilaya ya Kishapu, Nyabaganga Taraba alishuhudia mtanange huo akiwa ameambatana na viongozi wengine akiwemo, Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri hiyo, Stephen Magoiga Katibu Tawala Wilaya, Shadrack Kengese , Mkuu wa Polisi wilaya, SP.E.Ulomi na Mshauri wa Mgambo Wilaya,  SSgt.Charles Lyashimba.
 Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, Stephen Magoiga (kushoto) akibadilisha mawazo na mwenyekiti wa Bodaboda wilayani humo, Daniel Eva.
 Kocha wa Watumishi FC, Japhet Makelele akitoa mawaidha kwa wachezaji wake wakati wa kipindi cha mapumziko kwenye mchezo kati ya timu hiyo na Igaga FC.
 Mchezaji wa Watumishi FC mwenye namba 4 mgongoni akijaribu kuwatoka wachezaji wa Igaga FC huku wachezaji wenzake wakijiandaa kutoa msaada.
 Mkuu wa Wilaya ya Kishapu, Nyabaganga Taraba akizungumza na wananchi wa wilaya hiyo waliojitokeza katika uwanja wa shule ya msingi Mhunze kushuhudia fainali za kuwania kombe la ng’ombe kama shamrashamra za mbio za Mwenge wa Uhuru unaotarajiwa kuwasili wilayani humo Ijumaa ya Oktoba 7, 2016.
 Wananchi wa wilaya ya Kishapu wakishuhudia mtanange wa fainali hizo.
Mashabiki wa Watumishi FC wakishangilia ushindi wa timu yao mara baada ya kupigwa kwa mikwaju ya penati.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...