Na Eleuteri Mangi, MAELEZO
Watafiti wa masuala mbalimbali ya kijamii nchini wametakiwa kuhakikisha wanafanya tafiti ambazo zitawasaidia watu wenye ulemavu kupata vifaa saidizi ili waweze kumudu kuendesha maisha yao ya kila siku.
Hayo yamebainishwa na Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira na Watu wenye Walemavu Dkt. Possi Abdallah alipokuwa akizindua taarifa mpya ya utafiti inayobainisha hali halisi ya ulemevu na uzee nchini jijini Dar es salaam.
“Serikali inafarijika inapoona watu wanafanya utafiti ili kuwasaidia watu wenye ulemavu waweze kupata vifaa saidizi na ni kitu gani kifanyike ili NGOs ziweze kujikwamua kiuchumi na kuwasaidia wenye mahitaji” alisema Dkt. Possi.
Kuhusu suala la unyanyapaa kwa watu wenye ulemavu, Dkt. Possi amesema kuwa Ofisi ya Waziri Mkuu hapo tayari kuona wananchi wananyanyapaliwa huku akisisitiza kuwa watu wote ni sawa na ofisi hiyo ina “zero tolerance” kwa watu wanaowanyayapaa mlemavu.
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira na Watu wenye Walemavu Dkt. Abdallah Possi akiongea na wageni waalikwa hawapo pichani wakati wa uzinduzi wa taarifa mpya ya utafiti inayobainisha hali halisi ya ulemevu na uzee nchini jijini Dar es salaam.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...