Serikali kupitia Wakala wa Barabara Nchini (TANROADS), imeanzisha Kitengo maalum cha Wahandisi Washauri (TECU), ili kuwajengea uwezo wahandisi wazawa kusimamia miradi ya ujenzi wa barabara nchini na hivyo kuokoa kiasi kikubwa cha fedha ambacho kingetumika kuwalipa wahandisi washauri kutoka nje ya nchi. 

Akizungumza mkoani Geita mara baada ya kukagua mradi wa ujenzi wa barabara ya Uyovu-Bwanga-Biharamulo yenye urefu wa KM 112 ambayo pia inasimamiwa na Wahandisi Washauri Wazawa, Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa amesema mpaka sasa wahandisi wazawa wanasimamia miradi mbalimbali ya barabara katika mikoa ya Kagera, Mwanza, Geita na Kilimanjaro ambapo kupitia miradi hiyo serikali imeokoa dola za kimerani milioni mbili ambazo zingetumika kulipa wahadisi kutoka nje ya nchi. 

“Nitahakikisha ninakijengea uwezo kitengo hiki ili kuweza kuokoa fedha nyingi zaidi. Nimeridhishwa na usimamizi wa wahandisi hawa katika barabara hii ambayo ipo katika hatua nzuri”, amesema Prof Mbarawa. 

Waziri Mbarawa ameongeza kuwa Serikali itahakikisha kuwa miaka mitano ijayo miradi yote mikubwa nchini itasimamiwa na Wakala huo ili kuokoa fedha za ndani na badala yake fedha hizo kuelekezwa kwenye miradi mingine ya ujenzi. 
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa, akitoa maelekezo kwa Mkuu wa Kivuko cha MV. Chato, Eng. Fredinand Mishamo (Wa kwanza kushoto), alipokagua kivuko hicho, wilayani Chato, mkoani Geita. 
Fundi wa Kivuko cha Mv Chato kutoka Wakala wa Ufundi na Umeme Nchini (TEMESA), Bw. Mbondo Jackson, akimweleza Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa, namna injini ya Kivuko cha MV. Chato inavyotumia mafuta, alipotembelea kivuko hicho, wilayani Chato, Geita. 
Muonekano wa Kivuko cha MV Chato kilichopo Wilaya ya Chato mkoani Geita.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...