Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na
Mkewe Mery Majaliwa wakimsalimia Bahati Omary kutoka kijiji cha Nangao
Wilaya Liwale ambaye amejifungua mtoto wa kike katika Hospitali ya
wilaya ya Nachingwea Waziri mkuu alifika katika Hospitali hapo kujionea
jinsi huduma za afya zinavyo tolewa kwa wagonjwa waziri mkuu yupo
katika ziara ya kikazi katika wilaya ya Nachingwea na Ruwangwa Mkoani
Lindi
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa
akiongea na watumishi wa Hospitali ya Nachingwea pamoja na wananchi
waliofika katika Hospitali ya nachingwea Waziri Mkuu alifanya ziara ya
kutembelea hospitalini hapo kwa ajili yakuona na kusikiliza wagonjwa
wanavyo pata huduma
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa
akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Liwale Sarah Chiwanga ambaye
nimiongoni wa viongozi wa mkoa wa Lindi waliofika katika kiwanja cha
ndege Nachingwea kumpokea Waziri mkuu na mkewe Mary Majaliwa na kushoto
ni Mkuu wa Mkoa wa Lindi Godfrey Zambi ambao wamewasili katika Mkoa wa
Lindi kwa ziara ya kikazi katika wilaya ya Nachingwea na Ruwangwa
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...