Na: Genofeva Matemu –
WHUSM
Ushirikiano wa Kidiplomasia
kati ya Tanzania na China katika nyanja mbalimbali zikiwemo za Sanaa na Utamaduni
umekuwa chachu kubwa katika kuwajengea uwezo wasanii wetu na kutekeleza
shughuli za kimaendeleo zinazofanywa na wataalamu kutoka pande hizi mbili.
Hayo yamesemwa na
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye alipokua
akizindua wiki ya Maonyesho ya Utamaduni wa China katika Ukumbi wa Utamaduni wa
watu wa China leo jijini Dar es Salaam.
“Kwa miaka mingi Tanzania na China zimekuwa na
ushirikiano uliotoa fursa kwa watu wake kujifunza shughuli za sanaa na
kiutamaduni zilizoko katika kila nchi hivyo kuendeleza na kuuenzi ushirikiano
uliopo katika sekta za Sanaa na Stamaduni” amesema Mhe. Nnauye
Mhe. Nnauye amesema
kuwa ushirikiano wa nchi hizi mbili umeweza kukua, kuboresha na kuendeleza wasanii
wetu hasa katika kipindi hiki cha maonyesho ambapo hutoa nafasi kwa wasanii wa
Tanzania kujifunza mambo mbalimbali ya kiutamaduni na kuwapa wasanii wa hapa
nchini fursa ya kufanya maonyesho kama haya nchini China.
Kwa upande wake Kaimu
Balozi wa China nchini Tanzania Bw. GOU Haodong amesema kuwa Maonyesho ya Utamaduni
wa China hapa nchini yanatoa fursa nzuri kwa wananchi wa Tanzania kuelewa na
kujifunza utamaduni na sanaa ya China, kuimarisha ushirikiano wa utamaduni wa
China na Tanzania pamoja na kukuza urafiki wan chi hizi mbili.
Naye Mkurugenzi
Msaidizi Idara ya Utamaduni kutoka Jiangxi China Bw. Chen Hongmin amesema kuwa China
itaendelea kushirikiana na Tanzania katika kubadilishana uzoefu kwa sekta ya
Sanaa na Utamaduni na kujifunza mambo mapya ili kuendeleza Utamaduni,
ushirikiano na uhusiano wa kidiplomasia kati ya nchi hizi mbili.
Wiki ya Maonyesho ya
Utamaduni wa China itakuwa na maonyesho mbalimbali kama vile maonyesho ya
sarakasi ya Kichina, maonyesho ya picha, hadhara za opera za China, Udaktari wa
kijadi wa China na Utamaduni wa mazoezi maalumu yanayojenga afya yaitwayo
Qigong.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye (kushoto) akikagua picha mbalimbali za kiutamaduni wa China wakati wa uzinduzi wa Maonyesho ya Utamaduni wa China leo Jijini Dar es Salaam. (katikati mbele) ni Kaimu Balozi wa China nchini Tanzania Bw. GOU Haodong.
Kikundi cha Utamaduni na Sanaa cha Jiangxi kikionyesha sarakasi wakati wa uzinduzi wa Maonyesho ya Utamaduni wa China leo Jijini Dar es Salaam.
Kaimu Balozi wa China
nchini Tanzania Bw. GOU Haodong (kulia) akiteta jambo na Waziri wa Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye alipokua akikagua picha
mbalimbali za kiutamaduni wa China wakati wa uzinduzi wa Maonyesho ya Utamaduni
wa China leo Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkuu wa Kituo cha Utamaduni cha
China nchini Bw. GAO Wei.
Kaimu Balozi wa China
nchini Tanzania Bw. GOU Haodong (kulia) akiteta jambo na Waziri wa Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye alipokua akikagua picha
mbalimbali za kiutamaduni wa China wakati wa uzinduzi wa Maonyesho ya Utamaduni
wa China leo Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkuu wa Kituo cha Utamaduni cha
China nchini Bw. GAO Wei.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...