WENYEVITI wa Halmashauri ya wilaya ya Ilala Mkoani Dar es Salaam wamekutana Wilayani Bagamoyo katika Semina maalum ya kujengeana uwezo na uwelewa ikiwamo kutambua majukumu yao kwa lengo la kuepusha migongano kati ya Wenyeviti,Watedaji ,pamoja na Madiwani.

Akizungumza wilayani humo mara baada ya kufungua semina hiyo Mwenyekiti wa Wenyeviti mkoa wa Dar es Salaam ambaye pia ni Mwenyekiti wa wenyeviti Wilaya ya Kinondoni Juma Zubery alipongeza hatua ya wenyeviti wa wilaya ya Ilala kuona kuna umuhimu wa kufanya semina ya kukumbusha na kuelekezana majukumu ya weyeviti katika mitaa mbalimbali ili kuepusha migongano kati yao na watendaji wengine wa Serikali.

Zubery alisema uendeshaji wa Serikali za mitaa unachangakubwa ,ikiwamo viongozi wengi kushindwa kujuwa mjukumu yao hali inayosababisha kutoautiana mara kwa mara miongoni mwao nakudai kwamba mtendaji wa mtaa na mwenyekiti wanafikia hatua ya kugombea hata mihuli jambo ambalo kimsingi linatokana na uelewa mdogo wa kutojuwa mipaka ya kazi zao.

Kwaupande wake Menyekiti wa Wenyeviti katika Manispaa ya Ilala Ubaya Chuma aliwataka wenyeviti hao kuogoopa kutumia mihuli ya watendaji wa mtaa huku akidai kufanya hivyo ni kwenda kinyume cha sharia na kwamba kufanya hivyo nikukaribisha migongano miongoni mwao. 

Katika Semina hiyo wenyeviti zaidi ya 44 kutoka Halmashuri hiyo wamekutana huku wakimomba Mkuu wa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam kuona umuhimu wa kuandaa mafunzo kama hayo kwa wenyeviti wote wa Serikali za mitaa kwa mkoa wa Dar es Salaam.



Mwenyekiti wa Wenyeviti wa Serikali za mitaa mkoa wa Dar es Salaam Juma Zubery Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kufungua Semina elekezi kwa wenyeviti wa Serikali za Mtaa wilaya ya Ilala ambapo lengo la semina hiyo ilikuwa ni kuwajengea uwezo na uwelewa juu ya majukumu yao.
Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Mogo, Geoge Mtambalike akitoa mada ya ulinzi na usalama katika semina hiyo ya wenyeviti wa serikali ili kujuwa namna ya kuweza kukabiliana na vitendo vya kiarifu katika mitaa yao.
Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za mitaa wilaya ya Ilala, Ubaya Chuma akiwasilisha mada mbele ya wajumbe ambao ni wenyeviti wa Serikali za mitaa mbalimbali wilayani humo ambapo alijikita katika kutoa elimu ya kutambua majukumu yao nakuacha kumbea mihuri huku akidai ni makossa Mwenyekiti wa serikali ya mtaa kuchukua mhuhuri wa mtendaji wa mtaa au kata.
Wenyeviti wa Serikali za mitaa mbalimbali kutoka Halmashauri ya wilaya ya ilala wakisikiliza kwa makini mada ambayo ilikuwa ina tolewa na mtoa mada,Ubaya Chuma kuhusu wenyeviti hao kuona kwamba wanajukumu kubwa la kulinda usalama wa maeneo yao ikiwa pamoja na kuimarisha vikundi vya ulinzi na usalama. 
Katibu Tawala wilaya Bagamoyo Mjini Doris Mwakitobe akizungumza jambo wakati wakufunga semina ya wenyeviti wa serikali za mitaa mbalimbali wilaya ya Ilala,ambapo katika kufunga semina hiyo aliwataka kwenda kutumia mafunzo hayo kufanya kazi kwa bidi na kwa kuzingatia kauli mbiuya rais ya Hapa kazi tu kulia ni Mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa mogo Geoge mtambalike.Picha zote na Emmanuel Massaka,Globu ya Jamii.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...