KAMPUNI ya
Woolworths yenye maduka yakuuza nguo katika majiji ya Dar es Salaam na Arusha,
imemkabidhi Waziri Mkuu Kasim Majaliwa hundi yenye thamani ya shilingi milioni
20 ikiwa ni mchango wake kwa waathirika wa tetemeko la ardhi lililoukumba mkoa
wa Kagera.
Akizungumza
wakati akipokea hundi hiyo, Waziri Mkuu aliishukuru kampuni hiyo kwa msaada
walioutoa kwa watu walioathirika na tetemeko hilo ambalo lilisabisha vitu na
uharibifu mkubwa wa mali mkoani Kagera.
Waziri mkuu
alisema makampuni na biashara zinao mchango mkubwa katika kusaidia jamii na
kuisufu kampuni ya Woolworths ambayo alisema amekuwa akisikia kupitia vyombo
vya habari ikisaidia jamii zenye mahitaji.
“Napenda
kuishukuru kampuni ya Woolworths kwa kuguswa na tatizo lililowapata ndugu zetu
wa Kagera na kuona umuhimu wa kutoa mchango huu. Kampuni hii ni mfano wa
kuigwa kwa kuwa pamoja na kusaidia jamii pia imekuwa ikiuza nguo zenye ubora,” alisema.
Kwa upande
wake Mkurugenzi Mkuu wa wa kampuni hiyo Joehans Bushiri alimwambia Waziri Mkuu
kuwa, ni utaratibu wa kawaida wa kampuni hiyo kutenga sehemu ya faida yake kwa
ajili ya kusaidia jamii yenye uhitaji.
“Woolorths
imekuwa mstari wa mbele katika kusaidia jamii zenye mahitaji kama yatima na
makundi mengine. Msaada huu wa leo ni sehemu ya utaratibu tuliojiwekea kwa
ajili ya kurudisha sehemu ya faida tunayopata kwa jamii zenye mahitaji maalum,”
alifafanua.
Kampuni ya
Woolworths ni moja ya makampuni makubwa Africa na duniani yanayojihusisha na uuzaji wa nguo na vitu vya aina
mbali mbali vyenye ubora wa hali ya juu ikiwa na matawi mawili jijini Dar es
Salaam na matawi mawili jijini Arusha.
Waziri Mkuu Kasim Majaliwa (wa kwanza kushoto) akimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya Woolworths Tanzania Joehans Bushiri allipokuwa akitoa mchango wa hundi ya shilingi 20m/- ikiwa ni mchango wa kuchangia waathirika wa tetemeko mkoani Kagera. Walio kaa kulia ni Waziri wa Viwanda Biashara Charles Mwijage, Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Mwinyi Mvua na wa mwisho kulia ni Mkuu wa kitengo cha fedha wa kampuni hiyo Samson Katemi.
Waziri Mkuu Kasim Majaliwa (wa kwanza kushoto) akipokea mfano wa hundi ya shilingi 20m/- kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya Woolworths Tanzania Joehans Bushiri ikiwa ni mchango wa kuchangia waathirika wa tetemeko mkoani Kagera. Wengine ni Mkuu wa kitengo cha fedha wa kampuni hiyo Samson Katemi na Waziri wa viwanda Biashara Charles Mwijage.
Waziri Mkuu Kasim Majaliwa (wa kwanza kushoto) akipokea mfano wa hundi ya shilingi 20m/- kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya Woolworths Tanzania Joehans Bushiri ikiwa ni mchango wa kuchangia waathirika wa tetemeko mkoani Kagera. Wengine ni Mkuu wa kitengo cha fedha wa kampuni hiyo Samson Katemi na Waziri wa viwanda Biashara Charles Mwijage.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...