Meneja Uhusiano wa Kampuni ya Airtel Tanzania, Jackson Mmbando (kushoto) akimueleza jambo Mkuu wa wilaya Lindi, Shaibu Ndemanga (wapili kulia) juu huduma zitakazotolewa na mnara wa Airtel uliojengwa katika kijiji cha Cheleweni mara baada ya kuzindua mnara huo. katikati ni Meneja Mauzo wa Airtel Mkoa wa Lindi, Saleh Safy. Airtel imejenga mnara huo ambao utatoa mawasiliano katika vijiji vya Ng’apa ngapa, Cheleweni, Nchee, Nantumbya, Nanyuru pamoja na maeneo yanayowazunguka vijiji hivyo. Airtel imezindua huduma hiyo ili kuboresha , huduma za kifedha kwa njia ya mtandao Airtel Money na kuwaweza wananchi wa Lindi kupata mawasiliano ya uhakika katika kuendesha shughuli zao za kila siku kiuchumi na kijamii.
Mkuu wa Wilaya Lindi, Shaibu Ndemanga akizungumza na wananchi wakati wa uzinduzi wa mnara wa Airtel utakaotoa huduma ya mawasiiano katika vijiji vya Ng’apa ngapa, Cheleweni, Nchee, Nantumbya, Nanyuru pamoja na maeneo yanayowazunguka vijiji hivyo. anaefuata ni diwani wa viti maalum Lindi Bi, Somoe Pamui na Meneja Mauzo wa Airtel Mkoa wa Lindi, Saleh Safy. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...