Na Rashid Nchimbi wa Jeshi la Polisi Arusha

Katika kipindi cha toka Januari mpaka Oktoba mwaka 2016 ajali za vifo zimepungua kwa asilimia ishirini na nne ukilinganisha na kipindi kama hicho mwaka 2015, ambapo kulikuwa na jumla ya ajali za vifo 74 tofauti na mwaka huu kumekuwa na ajali 56 ambapo ni sawa na upungufu ya ajali 18 ambazo ni 24% .

Akitoa takwimu hizo katika sherehe za uzinduzi ya wiki ya nenda kwa Usalama Barabarani zilizofanyika katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Mkuu wa kikosi cha Usalama Barabarani mkoani hapa Mrakibu Mwandamizi wa Polisi (SSP) Nuru Kacharia alisema kwamba katika ajali hizo 74 kwa mwaka 2015 jumla ya watu 97 walipoteza maisha na mwaka huu 2016 kwa kipindi kama hicho ajali hizo ni 56 ambazo zilisababisha vifo vya watu 68.
Askari wa Kikosi cha Usalama Barabarani Koplo Athilio Choga akimuelezea mgeni rasmi mkuu wa wilaya ya Arusha Mh. Gabriel Daqarro (Mwenye suti) namna ya mpangalio wa mji unavyoweza kupanua barabara ili kuepukana na ajali.

Kacharia aliendelea kubainisha kwamba, mbali na upungufu wa ajali za vifo lakini kikosi hicho cha Usalama Barabarani kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wameweza pia kupunguza ajali za majeruhi kwa 5% ambapo mwaka 2015 kuanzia Januari hadi Oktoba ajali zilizosababisha majeruhi zilikuwa 763 tofauti na ajali zilizosababisha majeruhi 725 kwa kipindi kama hicho kwa mwaka huu wa 2016.

“Asilimia 75 ya ajalli za barabarani zinasababishwa na wanadamu kwa kutotii sheria za barabarani, madereva kuendesha vyombo vya usafiri wakiwa walevi, kuendesha kwa mwendokasi, watembea kwa miguu na waenda mikokoteni kutofuata sheria”. Alifafanua Mkuu huyo wa Usalama Barabarani.

Alisema mbali na makosa ya kibinadamu lakini pia, ubovu wa vyombo vya usafiri kama vile uchakavu wa magurudumu na kadhalika husababisha ajali kwa asilimia kumi na tano pamoja namiundo mbinu ya barabarainachangia kwa asilimia kumi.
Mkuu wa kikosi cha Usalama Barabarani mkoa wa Arusha (SSP) Nuru Kacharia akitoa takwimu juu ya hali ya usalama barabarani kwa wananchi wa Arusha wakati wa uzinduzi ya wiki ya nenda kwa usalama barabarani iliyofanyika jana katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha.

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Eng. Nuru umekuwa mzee hivi. Big up pia unga huo. Wakati haumuachi mtu.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...