WATANZANIA takribani asilimia 40 wanatakiwa wawe wamejiingiza kwenye uchumi wa viwanda mpaka kufikia 2020 ili kuweza kusaidia kukuza ajira za vijana na kuifanya Tanzania kuwa kwenye uchumi wa kati kwa maendeleo ya jamii na nchi kwa ujumla. 

 Akizungumza hayo wakati wa ufunguzi wa mkutano wa mwaka wa nne wa Taasisi isiyo ya kiserikali inayotoa msimbomilia (Barcode) za bidhaa (GS1) Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Bw. Charles Mwijage amesema kuwa Serikali imeazimia kufikisha asilimia 40 ya watanzania kufanya shughuli za uchumi wa viwanda kufikia 2020.

 “Tunataka mpaka kufikia 2020 watanzania takribani asilimia 40 wawe wamejikita kwenye uchumi wa viwanda ili kusaidia kukuza ajira kwa vijana na kuifanya Tanzania kuwa kwenye uchumi wa kati kwa maendeleo ya jamii nan chi yetu kwa ujumla” alisema Waziri Mwijage.

 Aidha Waziri Mwijage amesema kuwa Uchumi wa viwanda unatakiwa kukua nchini kuwezesha kuzalisha bidhaa bora zitakazouzwa ndani na nje ya nchi ili kukusanya kodi kwa ajili ya kupata huduma bora za kijamii kwa maendeleo ya wananchi wa Tanzania . 
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Bw. Charles Mwijage akiongea na wadau mbalimbali wa biashara kuhusu umuhimu wa kulipa kodi na kutumia msimbomilia(barcode) hawapo pichani wakati wa ufunguzi wa mkutano wa mwaka wa nne wa Taasisi isiyo ya kiserikali inayotoa msimbomilia (Barcode) za bidhaa (GS1) uliofanyika jijini dar es salaam.

Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Bw. Charles Mwijage wa pili kulia akikata keki kuadhimisha mwaka wa nne wa Taasisi isiyo ya kiserikali inayotoa msimbomilia (Barcode) za bidhaa (GS1) uliofanyika jijini dar es salaam wa kwanza kulia ni Mwenyekiti wa bodi ya GS1 Bw. Gideon Mazara.
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Bw. Charles Mwijage kulia akimpa mkono wa pongezi Afisa Mkuu wa elimu kwa mlipa kodi kutoka Mamlaka ya Mapato Nchini (TRA) kwa kudhamini mkutano wa mwaka wa nne wa Taasisi isiyo ya kiserikali inayotoa msimbomilia (Barcode) za bidhaa (GS1) uliofanyika jijini Dar es salaam.
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Bw. Charles Mwijage kushoto akipokea zawadi kutoka kwa mwakilishi wa kampuni ya Shea illushion kulia wakati wa ufunguzi wa mkutano wa mwaka wa nne wa Taasisi isiyo ya kiserikali inayotoa msimbomilia (Barcode) za bidhaa (GS1) uliofanyika jijini dar es salaam. Na Mpiga picha Wetu . Dar es salaam.

HABARI ZAIDI SOMA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...