BANK OF AFRICA- TANZANIA leo imezindua aina mpya ya mkopo wa ujenzi wa nyumba unaoitwa ‘WEZESHA’ ambapo mtu anaweza kukopa kiasi cha shilingi milioni 40 hadi 500 kwa mrejesho wa miaka hadi 25 bila utaratibu wa kutoa malipo yoyote ya awali.

Akizungumzia progamu hiyo, Naibu Mkurugenzi wa BANK OF AFRICA- TANZANIA bwana Wasia Mushi alisema, ‘programu hii ya mkopo wa ujenzi wa makazi mapya unawapa uwezo wateja wetu kubuni nyumba zao kadiri wanavyopenda, kulingana na mahitaji yao na ndani ya bajeti zao. Kwa kiwango kidogo kabisa cha riba na katika viwango vya punguzo, Bank ya Afrika pia imetengeneza mazingira rafiki na kuondoa usumbufu kwa mteja pindi anapohitaji mkopo huu’

Aidha, huduma ya mkopo ya ‘Wezesha’ inapatikana kwa watu wote wenye mishahara katika sekta za umma na binafsi, na kwa kutoa muda wa miaka 25 ya kulipa deni, mkopaji atapata uhuru zaidi pindi atakapochukua mkopo. 

Mpango wa huu wa ‘Wezesha’ kujenga makazi unalenga kutoa suluhu kwa changamoto za makazi zinazowakabili watanzania wengi ambao kwa mazingira ya kawaida hutumia zaidi ya miaka 10-15 kujenga nyumba ya kawaida ya kuishi. 
Kutoka kushoto ni Ibrahim Samuel- Meneja Uhusiano- Mikopo ya Nyumba, Wasia Mushi- Naibu Mkurugenzi Benki ya Afrika Tanzania (BOA), na Muganyizi Bisheko- Meneja Masoko Utafiti na Maendeleo wakiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani).
Kutoka kushoto ni Beatrice Mirigo- Marketing executive, Ibrahim Samuel- Meneja Uhusiano- Mikopo ya Nyumba, na Wasia Mushi- Naibu Mkurugenzi Benki ya Afrika Tanzania (BOA) wakiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...