Na Dotto Mwaibale

TAASISI ya Kifedha ya Bayport Tanzania juzi iliadhimisha miaka 10 tangu kuanzishwa kwake na kuelezea mafanikio makubwa iliyopata ndani ya kipindi hicho.

Akizungumza katika hafla hiyo iliyofanyika Hyatt Regency Hotel jijini Dar es Salaam juzi, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Bayport Tanzania, John Mbaga alisema ndani ya miaka 10 wameweza kupiga hatua kubwa kwa kuwafikia wananchi wengi.

"Tumepiga hatua kubwa kwa kuwafikia wananchi wengi ambao wamenufaika na huduma zetu" alisema Mbaga.Alisema kupitia taasisi hiyo wananchi wameweza kuanzisha biashara na kujenga nyumba ikiwa ni pamoja na kusomesha watoto.

Mgeni rasmi wa hafla hiyo Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angella Kairuki alisema Serikali inaipongeza taasisi hiyo kwa huduma za mikopo inayotoa kwa wananchi hivyo kusaidia kuinua pato la taifa na mtu mmoja mmoja.

"Changamoto kubwa iliyopo ambayo mnapaswa kuiangalia ni riba kubwa katika mikopo yenu jaribuni kuliangalia jambo hilo kwa karibu" alisema Kairuki.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angella Kairuki akihutubia katika hafla ya kutimiza miaka 10 ya Taasisi ya kifedha ya Bayport Tanzania iliyofanyika Hyatt Regency Hotel jijini Dar es Salaam juzi.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Bayport Tanzania, John Mbaga akizungumza kwenye hafla hiyo.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angella Kairuki (kulia), Mjumbe wa Bodi ya Bayport Tanzania, Mama Anna Mkapa (katikati) na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Bayport Tanzania, John Mbaga, wakikata keki katika maadhimisho ya miaka 10 tangu kuanzishwa kwa Bayport Tanzania yaliyofanyika Hyatt Regency Hotel Dar es Salaam juzi.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Bayport Tanzania, John Mbaga (kushoto), akimlisha keki Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Ali Hapi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...