Bendi ya muziki wa dansi ya C-Park Sound ya Kinondoni, Dar es Salaam imeendelea kutawala anga la muziki huo vitongoji vyote vya jiji ambapo mwishoni mwa wiki iliyopita ilidhihirisha kuwa ni moto wa kuotea mbali.

Jumamosi iliyopita, katika baa maarufu ya C-Park (zamani Matema) gazeti hili, lilishuhudia mamia ya mashabiki wakiburudika na muziki wa bendi hiyo huku wakisifu na kupiga makofi mara kwa mara kutokana na kuguswa mitima yao.

“Bendi hii kiboko, yaani siamini watu wote hawa wanaifuata bendi hii tu, au kuna promosheni hapa? Sio rahisi baa kujaza watu hivi wakati leo kumbi maarufu za Kinondoni nyingi ziko tupu. Kwa kweli nimewavulia kofia hawa vijana wa C-Park Sound,” akasema mpenzi mmoja anayejiita Lukaku.

Kiongozi wa bendi hiyo, Magazine, ameliambia gazeti hili kuwa, kujaza watu, kushangiliwa sana na kutuzwa pesa na zawadi nyingine ni kitu cha kawaida kabisa kwa bendi yake kwa hiyo hashangazwi na matukio ya aina hiyo.

“Tunajua nini tunafanya. Kila wiki tuko hapa baa ya C-Park, Kinondoni B, tunapiga muziki aina zote, tena kwa ubora wa asilimia mia moja. Hatubahatishi, kila anayekuja hapa huja tena na tena,” akajinasibu Magazine. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...