Na Is-haka Omar, Zanzibar.

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar  kimewataka Viongozi na Watendaji wa Jumuiya ya Umoja wa Wanawake  CCM (UWT) Tanzania  kuongeza juhudi katika kuimarisha Chama ili kiweze kushinda na kuendelea  kuongoza dola katika Uchaguzi Mkuu ujao.

Rai hiyo imetolewa na Katibu wa Idara ya Organazesheni Afisi Kuu Zanzibar, Nd. Haji Mkema wakati akizungumza na Watendaji wa Jumuiya hiyo kwa ngazi za Mikoa na Wilaya za Unguja Kichama katika ziara ya kuimarisha uhai wa Chama katika jumuiya hiyo.  

Alisema jumuiya hiyo inatakiwa kuandaa mapema mipango endelevu ya kuimarisha chama kwa kuongeza wanachama wapya ndani ya chama na Jumuiya  kwa lengo la kufanikisha ushindi wa CCM wa mwaka 2020.

Nd. Mkema alieleza kwamba lengo la ziara hiyo ni kuwakumbusha viongozi na watendaji wa UWT, majukumu ya msingi yanayotakiwa kufanyiwa kazi kwa haraka ili kuhakikisha CCM inaendelea kubaki na hadhi yake ya kusimamisha Dola inayojali misingi ya Demokrasia, Haki na utawala wa kisheria.

“ Chama Chetu kinajivunia kuwa na jumuiya imara ya Akina Mama ambayo imekuwa mstari wa mbele kutetea na kupigania maslahi ya CCM bila ya hofu katika mapambano ya Kisiasa nchini, na kupata ushindi wa kishindo unaotokana na ridhaa halali ya wananchi”., alisema Mkema na kusisitiza kuwa  Watendaji wa jumuiya hiyo wanatakiwa kutafuta ufumbuzi wa kudumu juu ya kasoro ndogo ndogo zilizomo katika jumuiya hiyo ili kuongeza ustawi wa CCM kisiasa nchini.

 Alisema kwamba Akina Mama ndio nyenzo muhimu ya kisiasa kwa chama hicho hivyo wanatakiwa kuendea na harakati za kujenga ushawishi kwa akina Mama wenzao waliopo katika makundi na vyama mbali mbali kujiunga na Chama hicho.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...