Kampuni ya Tanzania Distilleries Limited (TDL) kupitia chapa yake ya ‘Valeur Superior
Brandy’, kwa kushirikiana na kampuni ya Vuvuzela Company Ltd, wanatangaza rasmi fainali ya shindano la “Valeur Comedy Nights” msimu wa pili, ambalo ni
shindano la kusaka vipaji vya sanaa ya uchekeshaji.
Fainali hiyo inatarajiwa kufanyika Jumamosi tarehe 19 Novemba 2016, Katika ukumbi
wa 40/40 Baa, Tabata ambapo kutakuwa na washiriki 18 waliopatikana kutoka katika
fainali za wilaya za mkoa wa Dar es Salaam. Mashindano haya ni kusaka mshindi wa
mkoa wa Dar es Salaam.
Akizungumuza na waandishi wa Habari, Meneja wa Kanda wa Mauzo na Usambazaji wa Kampuni hiyo, Mwesige Mchuruza alisema, “Msimu wa pili wa “Valeur Comedy Nights”
umeendelea kupokelewa vizuri na wateja wetu. Kutokana na kwamba huu ni msimu wa
pili, wateja wanalifahamu vizuri shindano hili na tumeona wacheheshaji wengi
wakijitokeza kushindana. Washirika wetu kutoka Kampuni ta Vuvuzela Company Ltd
kwa mara nyingine tena wametoa msaada mkubwa kwani wamewapa washiriki
mafunzo na kuwatayarisha kwa fainali hizi”.
Mashindano hayo yalianza Septemba 6, 2016 yakijumuisha zoezi la kusajili watu
kushiriki katika mashindano hayo.
Mchuruza aliendelea kusema mshindi wa ‘Valeur Comedy Nights’ atapata pesa
taslimu 2,000,000/= na mafunzo ya vitendo ya miezi 6 na Evans Bukuku katika kampuni
yake ya Vuvuzela Company Ltd.
Meneja Mauzo na Usambazaji Kinywaji cha Valeur kutoka
Kampuni ya TDL, Mwesigwa Mchuruza akimkabidhi Hundi ya
Shilingi Milioni Mbili Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya
Vuvuzela, Evans Bukuku ikiwa zawadi ya mshindi wa kwanza
kwa mshindi atakayepatikana katika fainali shindano la
kuchekesha linayolotarajiwa kufanyika jumamosi Oktoba
19,2016 Katika Bar ya 40/40 iliyoko Tabata jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Vuvuzela, Evans
Bukuku(kushoto) akizungumza na waandishi wa habari(hawapo
pichani) wakati wa kutangaza zawadi za washindi katika fainali
zinazotarajiwa kufanyika jumamosi Oktoba 19,2016 Katika Bar
ya 40/40 iliyoko Tabata jijini Dar es Salaam. Katikati ni Meneja
Mauzo na Usambazaji Kinywaji cha Valeur kutoka Kampuni ya
TDL, Mwesigwa Mchuruza.Kulia ni mshindi wa Mwaka jana,
Hussein Athuman.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...