Na Anthony John,Globu ya Jamii

Shirika lisilo la Kiserikali linalojihusisha na Elimu nchini, HAKI ELIMU limeishauri Serikali kuharakisha uundaji wa bodi ya kitaalamu ya Walimu ili kusaidia kuweka na kubaini viwango bora vya taaluma ya Ualimu.

Ushauri huo,umekuja baada mapema mwezi huu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na Ufundi kutoa waraka Na.5 wa Mwaka huu 2016 unaoleta Mabadiliko kadhaa katika program za Mafunzo ya Ualimu nchini.

Akizungumza na Waandishi wa Habari jijini Dar es salaam Mkurugenzi mtendaji wa shilika Hilo la HAKI ELIMU, John Kalage amesema miongoni mwa Mabadiliko hayo ni kwenda mamlaka ya usimamizi wa Elimu ngazi ya Cheti na stashahada kutoka NACTE na kuyarudisha wizarani chini ya uangalizi wa baraza la mitihani NECTA.

Kalage amesema kuwa kwamujibu wa waraka huo programu za Mafunzo ya Ualimu zitakuwa Astashahada Cheti, na stashahada , Diploma Mafunzo taraji ya stashahada ya juu ya Elimu sekondari yalikuwa yakitolewa kuanzia Mwaka wa masomo 2014/15 yamesitishwa.

"Wizara ya Elimu ndio itakuwa ikitoa maelezo ya sifa za kujiunga na Mafunzo ya Ualimu, Necta itakuwa inasimamia Mafunzo ya Ualimu huku ikitahini na kutoa tuzo", amesema Kalega.
Mkurugenzi Mtendaji wa Haki Elimu,John Kalage katikati akizungumza na Waandishi wa Habari juu ya kuishauri Serikali kuharakisha uundaji wa bodi ya kitaalamu ya Walimu ili kusaidia kuweka na kubaini viwango bora vya taaluma ya Ualimu.Kulia ni Meneja Habari na Utetezi-Haki Elimu,Elisante Kitulo,Kutoka Kushoto ni Maneja Udhibiti Ubora Haki Elimu,Robert Mihayo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...