Hospitali ya
Taifa Muhimbili imepokea msaada wa mashine
kubwa na ya kisasa ya Utra Sound maalum kwa ajili ya kuwahudumia wagonjwa wenye
matatizo ya Figo.
Msaada huo
umetolewa leo na Hospitali ya Chuo Kikuu
cha Haukeland cha nchini Norway ambapo pamoja na mambo mengine wameahidi
kuendelea kutoa ushirikiano katika
maeneo ya elimu , utafiti pamoja na vifaa tiba.
Daktari
Bingwa wa magonjwa ya Figo ambaye pia Mhadhiri kutoka MUHAS Paschal
Ruggajo amesema mashine hiyo itasaidia
kuchukua sampuli ya figo kwa ajili ya kugundua
magonjwa ya Figo , kuweka vifaa
kwenye mishipa damu kwa wagonjwa wanaoanzishiwa matibabu ya uchujaji wa damu na
kugundua matatizo mbalimbali ya Figo.
“ Kwa muda
mrefu sasa tumekua na ushirikiano wa karibu kati ya Hospitali hiyo , MUHAS na
MNH na wametusaidia kufundisha Madaktari
sita wa Figo , wameshatoa mashine za kusafisha Figo na sasa wametupatia mashine
hii kubwa ya Utra Sound kwakweli tunawashukuru kwa msaada wao.” Amesema Dk.
Ruggajo.
Akizungumza
kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili , Dk . Hedwiga
Swai ambaye ni Mkurugenzi wa Huduma za Tiba ameishukuru Hospitali hiyo ya
Haukeland na kusisitiza kuwa msaada huo
umekuja wakati muafaka kwakua mashine
hiyo itasaidia sana katika kitengo cha Figo.
Hii ndio
mashine ya Utrasound ambayo itatumika kuchukua sampuli
ya figo kwa ajili ya kugundua magonjwa
ya Figo , kuweka vifaa kwenye mishipa damu kwa wagonjwa wanaoanzishiwa
matibabu ya uchujaji wa damu na kugundua matatizo mbalimbali ya Figo.
Profesa
Einar Svastard ( kulia)
akimkabidhi msaada wa mashine
kubwa ya kisasa ya Utrasound Mkurugenzi
wa huduma za tiba MNH Dk. Hedwiga
Swai .
Profesa
Einar Svastard akimfanyia uchunguzi mgonjwa kwa kutumia mashine hiyo .
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...