Jaji Kiongozi, Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Ferdinand Wambali (wapilikushoto) akiwa ofisini kwa Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Meja Jenerali Mstaafu, Mhe. Salum Kijuu pindi alipomtembelea ofisi kwa Mkuu wa Mkoa huyo kumpa pole kufuatia tetemeko la ardhi lililotokea mkoani Kagera mnamo tarehe 10.09.2016 na kusababisha maafa katika baadhi ya miundombinu mkoani huo, Mahakama Kuu ikiwa mojawapo. Kulia ni Mhe. SalvatoryBongole, Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu- Kanda ya Bukoba.
Jaji Kiongozi, Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Ferdinand Wambali, (wa pili kulia) akikagua jengo la Mahakama Kuu, Kanda ya Bukoba ambalo lilipata mipasuko ‘minor cracks’ kufuatia tetemeko la ardhi lililotokea mkoani Kagera. Pamoja ni Jaji Kiongozi, wa pili kushoto ni Mhe. Jaji Matogoro, Jaji wa Mahakama Kuu, Kanda ya Bukoba, wa nne kushoto ni Mhe. Ilvin Mugeta, Msajili- Mahakama Kuu ya Tanzania ambaye aliambatana na Mhe. Jaji Kiongozi katika ziara yake Mkoani humo.
Jaji Mfawidhi, Mahakama Kuu Kanda ya Bukoba, Mhe. Salvatory Bongole, akiongea kitu mbele ya Watumishi wa Mahakama, Kanda ya Bukoba kabla ya kumkaribisha rasmi Mhe. Jaji Kiongozi kuongea na Watumishi wa Mahakama wa Kanda hiyo mara baada ya kukagua jengo la Mahakama lililopata maafa kufuatia tetemeko la ardhi.
Jaji Mfawidhi, Mahakama Kuu Kanda ya Bukoba, Mhe. Salvatory Bongole, akiongea kitu mbele ya Watumishi wa Mahakama, Kanda ya Bukoba kabla ya kumkaribisha rasmi Mhe. Jaji Kiongozi kuongea na Watumishi wa Mahakama wa Kanda hiyo mara baada ya kukagua jengo la Mahakama lililopata mipasuko kufuatia tetemeko la ardhi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...