Mtindo wa Karate wa Okinawa Goju Ryu shina la Jundokan So Honbu Tanzania linalo ongozwa na mkufunzi wake mwakilishi sensei Rumadha Fundi, kwa ushirikiano na uongozi wa dojo zote mbili, yaani Jamhuri na Zanaki linazidi kuwa imara chini ya uongozi wa wakilishi wa matawi makuu mawili ya mtindo huo wa Goju Ryu.
Ingawa ni dojo au shule mbili, lakini zote zina lengo moja tu kulitumikia jamii ya wana Goju Ryu Karate. Sensei Rumadha, alipata fursa yakuwa na mazoezi na shule hizi mbili na pia kuafikiana na wanafunzi waandamizi wa shule hizo na kuleta mabadiliko katika mbinu za ufundishaji, ikiwa pamoja na kushirikiana kwa mazoezi ya pamoja mara kwa mara kati ya dojo hizo.
Jundokan Zanaki Dojo.
Mtindo huu wa Okinawa Giju Ryu, uliletwa hapa nchini na mwasisi wa mtindo huu, Sensei Nantambu Camara Bomani mwaka 1973, na unaendelea kufundisha maadili, nidhamu na mbinu za kujilinda kama jinsi inavyo fundishwa kiasilia hivi sasa huko Okinawa, Japan.
Sensei Rumadha pia, ameleza kujitolea kutoa mchango wake katika shule hizo, ikiwa na kuzitembelea mara moja kila mwaka na kuwa na semina ikiwemo kufanya majaribio au “Mitihani” ya mikanda ya ngazi za juu na vilevile mafunzo ya utafiti utumiaji kata au “Bunkai” kwa wanafunzi wa ngazi ya kati na ya juu.
Sensei Rumadha alikaririwa akisema, alipokelewa kwa ukarimu na unyenyekevu katika dojo zote mbili na wanafunzi waandamizi na walimu pia. Senpai Yusuf Kimvuli, Senpai Abdul Waheed, Senpai Bilal, Senpai Mwinyimvua, Sensei Maulid Pambwe, Sensei Mwagala chini ya Jamhuri dojo, pia kwa upande wa Zanaki Sensei Melkia, Sensei Rashid Almas, Senpai Seif, na uongozi wote wa Zanaki dojo akiwemo Mohammed Murudker.
Jundokan Jamhuri Dojo
Mipango ipo njiani kujadili na kupendekeza wanafunzi watakao fanya mitihani ya mikanda mieusi mwakani baada ya idhini ya Kancho Yoshihiro Miyazato toka makao makuu ya mtindo huo huko Naha, Okinawa.
Mara tu baada ya mkufunzi mkuu wa Jundokan Tanzania, Sensei Rumadha Fundi atakapo hudhuria Kongamano”Jundokan European Gasshuku 2017 ” la kila mwaka mtindo wa Goju Ryu Jundokan So Honbu, utakao fanyika mjini Warsaw, Poland mwezi July na kupata ushauri toka kwa viongozi watakao kuja toka Okinawa, Japan akiwemo mwenye kiti wa chama hicho Kancho Yoshihiro Miyazato na washauri wake wakuu wa mbinu za juu wa Jundokan, Sensei Tetsu Gima na Sensei Tsuneo Kinjo.
Tanzania ni moja ya nchi pekee katika Afrika mashariki yenye wana Karate wa mtindo wa Goju Ryu wenye uzoefu wa mafunzo ya Karate kwa miaka mingi.
Sensei Rumadha na masenpai Waheed kushoto na senpai Yusuf Kimvuli .
Uongozi wa Jundokan Jamhuri Dojo na bendera yao toka Naha, Okinawa , Japan .
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...