Mtangazaji wa Kipindi cha THE MBONI SHOW kinachoandaliwa na Kampuni ya Chocolate Princes na kurushwa na TBC1, Mboni Masimba, akizungumza kwenye Kongamano la SAUTI YA MWANAMKE lililofanyika jana Gold Crest Hotel Jijini Mwanza.

Kongamano hilo lililenga kuwakutanisha wanawake Jijini Mwanza kupata elimu ya kujikwamua kiuchumi katika masuala mbalimbali ikiwemo biashara/Ujasiriamali pamoja na mahusiano katika ndoa.

Mboni alisema Kongamano hilo litakuwa likifanyika kila mwaka kama sehemu ya shukurani kwa watazamaji wa kipindi cha The Mboni Show katika kuwainua wanawake nchini ambapo wanawake mbalimbali waliofanikiwa kimaendeleo wanazungumza na kuwahamasisha wanawake wengine kimaendeleo.

Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana mkoani Mwanza,Mary Tesha, alipongeza kongamano hilo kutokana na elimu inayotolewa katika kumhamasisha mwanamke kimaendeleo ambapo aliwataka wanawake kuendelea kujiunga na vikundi vya kimaendeleo ili kuhakikisha wananufaika na mikopo kutoka halmashauri husika inayotokana na asilimia tano ya mapato yake pamoja na ahadi ya Rais Magufuli ya kutoa milioni 50 kwa kila kijiji/mitaa.
Na BMG
Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana mkoani Mwanza,Mary Tesha, alipongeza kongamano hilo kutokana na elimu inayotolewa katika kumhamasisha mwanamke kimaendeleo ambapo aliwataka wanawake kuendelea kujiunga na vikundi vya kimaendeleo ili kuhakikisha wananufaika na mikopo kutoka halmashauri husika inayotokana na asilimia tano ya mapato yake pamoja na ahadi ya Rais Magufuli ya kutoa milioni 50 kwa kila kijiji/mitaa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...