SABINUS PETER
KWEKA
30/12/ 1935 - 22/11/2004
Baba yetu mpendwa, leo umetimiza miaka
kumi na mbili (12) tokea siku ulipotuacha gafla bila ya kwaheri kutokana na
shinikizo la Damu (Stroke). Hatuna cha kusema ila tunabaki kushukuru tuu maana
ilimpendeza Bwana zaidi.
Baba, tunakukumbuka sana na bado
tunahuzunika hasa tunapokumbuka mapokezi yako ya upendo tulipokuwa tukija
nyumbani, ulitupenda sana hilo tunakiri ulipenda hata majirani waliokuzunguka,
ukiwapa ushauri na misaada mingi hata wakakuchagua kuwa Diwani wao na M/Kiti wa
Kanisa. Ulimpenda sana Mungu, hatukulala wala kuamka bila ya kuomba Rozari
ilikuwa nguzo yako kuu.
Ulipenda sana Elimu, ulipiga vita sana adui ujinga kwa
nguvu zako zote,ulitusomesha pamoja mshahara wako ulikuwa mdogo, tunatamani
sana ungekuwepo ufaidi hata matunda ya jasho lako hilo. Ulipenda sana tujue njia
mbadala za kupata kipato kingine kama
Kilimo, n.k. Maana ulisema mshahara tuu si kitu. Ulitufundisha biashara ili
tukikwama makazini tujue pa kukimbilia kweli ulikuwa Baba mfano mzuri wa
kuigwa.
Unakumbukwa
sana na sisi wanao JANE,
FESTO,EUGENIA,ELIZABETH, CECILIA na THADEI,
WAJUKUU NA VITUKUU, dadako wa pekee SR. DEVOTHA KWEKA CDNK, WAKWEKA wote wa NARUMU, Ndugu, na Marafiki wote.
Misa
ya kumuombea imefanyika leo Parokia ya Mkolani.
“Raha ya Milele
Umpe Eee Bwana…..”
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...