Madaktari Bingwa wa Moyo kutoka Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na Madaktari wenzao kutoka Taasisi ya Open Heart International (OHI) ya Nchini Australia wakitoa huduma ya matibabu ya moyo bila ya kupasua kifua (Catheterization) kwa mgonjwa. Kushoto ni Afisa Muuguzi Ayoub Mchau, akifuatiwa na Dkt. Daniel Maclennan na kulia ni Dkt. Peter Kisenge.
Afisa Muuguzi wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) Ayoub Mchau akiendelea na maandalizi ya kazi ya kutoa huduma ya matibabu ya moyo bila ya kupasua kifua (Catheterization) kwa mgonjwa huku Dkt. Daniel Maclennan (kulia) na Dkt. Peter Kisenge (katikati) wakimtazama. Taasisi hiyo kwa kushirikiana na Taasisi ya Open Heart International (OHI) ya Nchini Australia hivi sasa iko katika kambi maalum ya siku sita ya upasuaji kwa wagonjwa wa moyo na katika kambi hiyo wagonjwa 20 wanarajiwa kupata matibabu.
Dkt. Bingwa wa Moyo kutoka Taasisi ya Open Heart International (OHI) ya Nchini Australia akitoa elimu kwa vitendo jinsi ya upasuaji wa moyo bila ya kupasua kifua (Catheterization) kwa mgonjwa unavyofanyika. Taasisi hiyo kwa kushirikiana na Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) wako katika kambi maalum ya siku sita ya upasuaji kwa wagonjwa wa moyo ambapo kazi hiyo inaenda sambamba na utoaji wa elimu kwa wataalamu wa ndani wakiwemo madaktari, wauguzi, wagavi na mafundi wanaohusika na utengenezaji wa mashine za kimatibabu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...