MKE wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein, akisalimiana na Viongozi wa Dini wakati akiwasili katika ukumbi wa Chuo cha Amali Vitongoji Pemba, kuzungumza na Waumini wa Dini na kuzindua Albam la Kwaya ya R.G.C, ya Chakechake, Pemba.
MKE wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein, akiangalia bidhaa zinazotengenezwa na Kikundi cha Wawanawake cha Nia Njema cha Wete Pemba wakati wa mkutano huo na Viongozi wa Dini Kisiwani Pemba uliofanyika katika Ukumbi wa Chuo cha Amali Vitongoji
MKE wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein, akizungumza na Waumini wa Dini wa madhehebu mbalimbali ya Kikristo kisiwani Pemba wakati wa mkutano wake wa kuwashukuru kwa ushirikiano katika shughuli za maendeleo na kudumisha amani na kuwazinduliwa Albam ya Kwaya ya Kanisa la R.G.C Chakechake, uliofanyika katika ukumbi wa Chuo cha Amali Vitongoji Pemba. kulia Mke wa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mama Asha Suleiman na Mchungaji wa Kanisha la Anglikana Zanzibar Emanuel Masoud.
BAADHI ya Waumini wa madhehebu mbalimbali wa Dini ya Kikristo kisiwani Pemba wakimsikiliza Mke wa Rais wa Zanzibar akitowa nasaha zake kwa waumini hao katika ukumbi wa Chuo cha Mafunzo ya Amali Vitongoji Pemba
MKE wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein, akionesha Albam ya Kwaya ya R.G.C ya Chakechake baada ya kuinduwa ikiwa na nyimbo za kuitakia Amani Zanzibar uzinduzi huo umefanyika katika ukumbi wa Chuo cha Mafunzo ya Amali Vitongoji Pemba.(Picha zote na Othman Maulid)
Kwa taarifa kamili BOFYA HAPA
Kwa taarifa kamili BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...