Mbunge wa Jimbo la Rufiji Mohamed Mchengrwa akizungumza na umati wa wananchi wa kijiji cha Kilimani Kata ya Ngorongo Wilayani Rufiji Mkoa wa Pwani, katika mkutano maalumu wa dharula kwa ajili ya kurudisha hali ya amani na utulivu baada ya kutokea kwa watu wawili kupoteza maisha kufuatai mapigano ya wakulima na wafugaji.
NA VICTOR MASANGU, RUFIJI
WATU wawili wamepoteza maisha baada ya kutokea kwa vurugu kubwa na kusababisha mapigano baina ya jamii ya wafugaji na wakulima katika kijiji cha Kilimani kata ya Ngorongo Wilayani Rufiji Mkoani Pwani baada ya wafugaji hao kuamua kuingiza ng’ombe zao kinyume na sheria na taratibu zilizowekwa katika mashamba na kufanya uharibufu wa mazao.
Katika matukio hayo mawili ya mauaji ya kusikitisha imeelezwa kuwa yametokea juzi majira ya saa 2:30 za asubuhi baada ya mkulima mmoja aliyetambulika kwa jina la Mwidini Mpange (23)pamoja na Jugi Bushini (23) ambaye ni mfugaji walipoteza maisha kutokana na kuibuka kwa mapigano hayo ambayo yaliweza kuleta hali ya taharuki na hofu kubwa na uvunjifu wa amani kwa wananchi wa eneo hilo.
Kufuatia kutokea kwa mauaji hayo Tanzania daima imeweza kufika katika eneo la kijiji hicho na kuzungumza na Baba mdogo wa marehemu ambaye ni mkulima aliyejitambulisha kwa jina la Omary Mpange ambapo amesema mwanaye alipatwa na umauti baada kundi la wafugaji jamii ya wasukuma zaidi ya 50 waliamua kumvamia na kumshambulia kwa mikuki,masime pamoja na mapanga kisha kwenda kumtupa mashambani.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...