Na Nteghenjwa Hosseah - Arusha.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Mashaka Gambo amewataka wafadhili na wadau wa watoto kubuni miradi inayoendana na kusaidia  Mpango wa Serikali wa Elimu bure kwa shule za Msingi na Sekondari  ili kupunguza changamoto zinazojitokeza kwa sasa na kuuwezesha mpango huu kutekelezwa  kwa mafanikio makubwa.

Mhe. Gambo ameyasema hayo wakati wa Mkutano wa kushirikishana tuliojifunza wakati wa utekelezaji wa mpango wa pamoja tuwalee uliotekelezwa kwa miaka sita kwenye Kanda ya Kaskazini  na ambao kwa sasa umemaliza muda wake ulifanyika kwenye Hotel ya Mt Meru Jijini hapa.

Akizungumza katika Mkutano huo Mkuu wa Mkoa amesema kazi kubwa imefanyika wakati utekelezaji wote wa mradi  na mafanikio yake tumeonekana kwani watoto wamefikiwa na kusaidiwa kutoka katika mazingira hatarishi yaliyokuwa yanawakabili na wengine kupatiwa kadi za msamaha wa matibabu na zaidi mradi huu umekabidhiwa kwa Halmashauri husika ambazo  zitaendelea kusimamia na kutekeleza  mipango iliyowekwa chini ya mradi wa Pamoja Tuwalee.

Aliendelea kusema kuwa kukamilika kwa mradi huu katika awamu ya kwanza ni wazi kabisa kwamba ni maandalizi ya mradi mwingine ambao utakua na malengo yanayoshabihiana na programu ya awali hivyo ni vyema kwa kuwa walengwa bado ni watoto niwatake wadau kubuni miradi utakaolenga kusaidia Elimu bure na kwa kuwa watoto wote wanapata Elimu bure kupitia mpango huu basi ni vyema mkaelekeza nguvu kwenye utoaji wa Chakula kwa wananfunzi suala ambalo tumeona ni changamoto kwa watoto wetu.
   Mkuu wa Mkoa wa Arusha akizungumza na wadau wa Mkutano 

    Mkurugenzi wa WEI-TANZANIA Bi. Lilian Badi (aliyesimama) akielezea mafanikio ya Mradi wakati wa Mkutano wa kuhitimisha mradi wa Pamoja Tuwalee.
  Mkurugenzi Mkuu wa World Education Inc Bi.Gill Garb akitoa taaria ya utekelezaji wa mradi wa Pamoja Tuwalee kupitia WEI-Bantwana.
 Mwakilishi wa US-AID Tanzania Bi. Maria Busquets akielezea namna ambavyo Shirika lake limefanikisha utekelezaji wa mradi wa Pamoja Tuwalee.
 Mkurugenzi wa Kituo cha Maendeleo ya Wanawake, watoto na vijana (CWCD) Bi. Hindu Ally Mbwego akielezea mafanikio ya mradi kupitia Kituo chake ambao ndio watekelezaji katika Halmashauri za Jiji la Arusha, Karatu na Moshi.
Picha ya pamoja ni Mkuu wa Mkoa wa Arusha (katikati mbele), Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi waliotekeleza mradi huu, viongozi wa WEI, US AID, CWCD pamoja na  Wadau  wa watoto walioshirki katika Mkutano wa kuhitimisha mradi wa Pamoja Tuwalee.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...