BENDI saba za muziki
wa dansi zimethibitisha kushiriki mashindano ya Mtandao wa Wasanii Tanzania
(SHIWATA) na timu nane za soka za maveterani nazo kumekubali kumtafuta bingwa
wa mchezo huo.
Mwenyekiti wa
SHIWATA, Cassim Taalib alisema jana kuwa mashindano hayo ambayo yanashirikisha
michezo jingine ya mpira wa kikapu,Sarakasi,kun-fu na kaswida,mshindi wa kila
mchezo atakabidhiwa zawadi katika kijiji cha wasanii Mwanzega Mkuranga kwenye sherehe za kugawa nyumba Desemba mwaka huu.
Taalib alisema
mashindano ya soka yatafanyika Desemba 9 mwaka huu kwenye viwanja cha shule ya
Msingi Kitunda zikipambana timu za Kisarawe veterani, Stakishari veterani,
Vituka veterani, Mbagala veterani, Kigogo TZF, TBC veteran na wenyeji Kitunda
na Kivule veteran.
Alisema katika muziki
wa dansi bendi zilizothibitisha kushiriki ni Tanzania One Theatre (TOT),
Magereza Jazz (Mkote Ngoma), Mwenge Jazz (Panselepa),
Hisia Sound (Abdul
Salvador) JKT Kimbunga Stereo,Vijana Jazz na Wazee Sugu ya King Kikii ambazo
zitaoneshana umahiri wao kwenye kuimba na kupiga vyombo.
"Mpaka sasa
mashindano ya Kikapu yanayoshirikisha timu 16 za wanaume na nne za wanawake
yanaendelea viwanja vya ndani vya taifa.Timu hizo ni Kurasini Meat,Yellow
Jackets,Chui,Kijichi Worriors,Segerea BC, Jogoo,TMK Rockets,Oilers,
Hopper, TM Rockets, Chang'ombe,Montfort,"Timu za
wanawake ni Ukonga Queens,Vijana Queens,Ukonga Princesses na Oilers Princesses
ambazo bingwa atazawadiwa kikombe na
kukabidhiwa Kiwanja cha kujenga ofisi ya timu"alisema Taalib.
Alisema katika
mashindano ya kun-fu klabu zilizothibitisha kushiriki ni Begeja wu --shu,
Karakata Wu-shu na Kigogo Wu-shu ambazo zitapambana kwenye ujumbe as CCM
Mchikichini kwa mchezaji mmoja mmoja.
Naye msimamizi wa
mchezo as sarakasi,Selemani Penne
alisema maandalizi ya mashindano ya
mchezo huo yamekamilika na itavukutanisha vikundi vya Butterfly Arts
Group,Happy Center acrobatic, Black Lion na Jivunie.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...