BENDI saba za muziki wa dansi zimethibitisha kushiriki mashindano ya Mtandao wa Wasanii Tanzania (SHIWATA) na timu nane za soka za maveterani nazo kumekubali kumtafuta bingwa wa mchezo huo.


Mwenyekiti wa SHIWATA, Cassim Taalib alisema jana kuwa mashindano hayo ambayo yanashirikisha michezo jingine ya mpira wa kikapu,Sarakasi,kun-fu na kaswida,mshindi wa kila mchezo atakabidhiwa zawadi katika kijiji cha wasanii Mwanzega Mkuranga kwenye  sherehe za kugawa  nyumba Desemba mwaka huu.

Taalib alisema mashindano ya soka yatafanyika Desemba 9 mwaka huu kwenye viwanja cha shule ya Msingi Kitunda zikipambana timu za Kisarawe veterani, Stakishari veterani, Vituka veterani, Mbagala veterani, Kigogo TZF, TBC veteran na wenyeji Kitunda na Kivule veteran.

Alisema katika muziki wa dansi bendi zilizothibitisha kushiriki ni Tanzania One Theatre (TOT), Magereza Jazz (Mkote Ngoma), Mwenge Jazz (Panselepa),
Hisia Sound (Abdul Salvador) JKT Kimbunga Stereo,Vijana Jazz na Wazee Sugu ya King Kikii ambazo zitaoneshana umahiri wao kwenye kuimba na kupiga vyombo.

"Mpaka sasa mashindano ya Kikapu yanayoshirikisha timu 16 za wanaume na nne za wanawake yanaendelea viwanja vya ndani vya taifa.Timu hizo ni Kurasini Meat,Yellow Jackets,Chui,Kijichi Worriors,Segerea BC, Jogoo,TMK Rockets,Oilers, Hopper,  TM Rockets, Chang'ombe,Montfort,"Timu za wanawake ni Ukonga Queens,Vijana Queens,Ukonga Princesses na Oilers Princesses ambazo  bingwa atazawadiwa kikombe na kukabidhiwa Kiwanja cha kujenga ofisi ya timu"alisema Taalib.

Alisema katika mashindano ya kun-fu klabu zilizothibitisha kushiriki ni Begeja wu --shu, Karakata Wu-shu na Kigogo Wu-shu ambazo zitapambana kwenye ujumbe as CCM Mchikichini kwa mchezaji mmoja mmoja.




Naye msimamizi wa mchezo as  sarakasi,Selemani Penne alisema maandalizi ya  mashindano ya mchezo huo yamekamilika na itavukutanisha vikundi vya Butterfly Arts Group,Happy Center acrobatic, Black Lion na Jivunie.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...