Msajili wa Hazina, Bw. Lawrence N. Mafuru (Wapili Kulia) akifafanua jambo wakati wa Mkutano wa Mwaka wa Wenye Hisa wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) uliofanyika katika Ukumbi wa Benki hiyo.
Msajili wa Hazina, Bw. Lawrence N. Mafuru (Kulia aliyeinama) akisaini Kitabu cha Wageni wakati alipowasili kuhudhuria Mkutano wa Mwaka wa Wenye Hisa wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB). Wanaomtazama ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TADB, Bibi Rosebuld V. Kurwijila (Katikati) na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo, Bw. Francis J. Assenga (Kushoto).
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TADB, Bibi Rosebuld V. Kurwijila (Kushoto) akifungua Mkutano wa Mwaka wa Wenye Hisa wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) uliofanyika katika Ukumbi wa Benki hiyo.
Katibu wa Bodi ya Wakurugenzi ya TADB, Bibi Neema C. John (Kushoto) akisoma agenda za Mkutano wa Mwaka wa Wenye Hisa wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) uliofanyika katika Ukumbi wa Benki hiyo. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo, Bw. Francis J. Assenga.
Baadhi ya viongozi waandamizi wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) wakifuatilia Mkutano huo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...