Hapa
kazi tu ni kaulimbiu inayohamasisha watu kufanya kazi kwa bidii na kuzingatia
fursa mbalimbali zilizopo, usemi huu umetimia kwa Mama Paulina Kulwa mkazi wa
Mwanza baada ya kukabidhiwa kitita cha shilingi milioni mia moja kutoka kampuni
ya simu za mkononi ya Vodacom Tanzania kwa kushirikiana na Benki ya CBA.
Paulina
alikabidhiwa hundi hiyo katika ofisi za Vodacom jijini mwanza na Meneja Masoko
na huduma za Kifedha Vodacom Tanzania, Noel Mazoya na kusema lengo la kuanzisha
huduma hii ni kuwasaidia Watanzania kuwa na utamaduni wa kuweka akiba.
Bi Paulina Kulwa (Kulia) akikabidhiwa
hundi ya mfano wa Tsh Milioni 100 baada ya kuibuka mshindi katika promosheni ya
Jiongeze na M-Pawa
Bi Paulina Kulwa (Kulia) akiwa na pacha
wake katika duka la Vodacom City Mall jijini Mwanza katika hafla ya kumpongeza
na kumkabidhi hundi baada ya kuibuka mshindi katika promosheni ya Jiongeze na
M-Pawa
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...